• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MARA KUTOA ELIMU YA CHAKULA KILICHORUTUBISHWA MASHULENI

Posted on: June 1st, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bi. karolina Mthapula amewataka wajumbe wa kamati ya lishe pamoja na Elimu Mkoa wa Mara kuhakikisha kuwa elimu kuhusu urutubishaji  wa chakula inasambazwa kwa watoto mashuleni, waalimu, wazazi na wananchi wote kuanzia ngazi ya chini ili kuwepo na uelewa wa umuhimu wa kutumia chakula kilichorutubishwa kwani ni muhimu kwa afya ya watoto.

Bi. Mthapula ametoa kauli hiyo wakati akifungua kikao cha Kamati ya Lishe ya Mkoa pamoja kilichowashirikisha Maafisa Elimu kuhusu urutubishaji wa unga wa mahindi unaozalishwa na viwanda vidogovidogo na kati vilivyopo Mkoani Mara, kikao kilichofanyika leo tarehe 31 Mei2021 katika ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Ninaomba wajumbe na wataalamu mliopo hapa tuhakikishe kuwa elimu tunayoipata hapa tunaipeleka kwa  wananchi wote wa Mkoa wa Mara kwani suala la lishe ni suala muhimu kwa afya ya watoto wetu na linapelekea afya ya watoto kuimarika pamoja na kuongezeka kwa  kiwango cha ufaulu mashuleni”.

Aidha amewataka maafisa elimu kuongeza ufanisi katika kutoa elimu ya lishe mashuleni ili watoto wawe na uelewa stahiki ili nao waweze kwenda kupandikiza elimu hiyo majumbani na kwa jamii inayowazunguka.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Frolian Tinuga amesema kuwa Mkoa unaendelea kuweka mikakati madhubuti ikiwemo kukutana na wadau pamoja na wazalishaji kujadili namna bora ya utekelezaji wa mwongozo wa kitaifa wa utoaji wa chakula lishe kwa wanafunzi elimu msingi unatumika katika shule zote nchini.

“Kama Mkoa tumedhamiria kusimamia na kuhakikisha Muongozo wa lishe mashuleni unatekelezeka kwa kuhakikisha tunaendelea kuhamasisha, kutoa elimu na kuwajengea uwezo wazalishaji waweze kurutubisha vyakula wanavyozalisha sambamba na kuhakikisha wanafunzi wote mashuleni wanakula chakula kilichorutubishwa” alisema Dkt. Tinuga.

Kwa upande wake, mwakilishi wa ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bwana Steven Mtambi amesisitiza ulimaji na ulaji wa mahindi ya njano, maharage, viazi, mbogamboga na matunda kwa  shule zenye mazingira yanayowezekana kwani vyakula hivi vina virutubisho ya kutosha na vinasaidia kwa kiwango kikubwa kujenga afya ya watoto.

Bwana Mtambi ameeleza kuwa upungufu wa virutubisho unaweza kusababisha udumavu katika ukuaji wa watoto pamoja na matatizo ya watoto kuzaliwa na mgongo wazi na kichwa kikubwa.

“Asilimia 49% ya watu wa Mkoa wa Mara wana upungufu wa wekundu wa damu unaosababishwa na kukosa lishe bora hivyo nguvu ikiwekezwa katika kuwepo na huduma ya chakula na lishe kwa wanafunzi kutasaidia kuwajengea afya nzuri, kuongeza mahudhuri,kupunguza utoro,kuongeza kiwango cha ufaulu” alisema Bwana Mtambi.

Aidha akimkaribisha Katibu Tawala, Afisa Lishe Mkoa wa Mara Bwana Paul Makali amesema kuwa Mkoa umejipanga kuwajengea uwezo kamati za lishe za Halmashauri ili kuona namna bora ya kuondoa changamoto za lishe katika Mkoa wa Mara.

Bwana Makali amevitaja vyakula vinavyotakiwa kurutubishwa kuwa ni chumvi, mafuta ya kula, unga wa mahindi pamoja na unga wa ngano.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa