• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara kupigania Chuo Kikuu kuanza haraka

Posted on: July 25th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameeleza kuwa Mkoa wa Mara utachukua hatua za maksudi kuhakikisha Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere cha Sayansi na Teknolojia kinaanza kudahili wanafunzi mapema iwezekanavyo.

Mheshimiwa Hapi ameeleza hayo katika ziara yake aliyoifanya leo tarehe 19 Julai 2021 katika Chuo hicho kukagua maendeleo ya miradi inayotekelezwa na Chuo hicho.

“Kuanza kwa Chuo hiki na hii idadi ya wanafunzi inayotegemewa inaweza kubadilisha kabisa maendeleo ya Mkoa wa Mara ndani ya muda mfupi kwani vyuo vikuu vimekuwa kama kichocheo cha uchumi katika mahali vilipo” ameeleza Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameahidi kuandaa safari maalum pamoja na viongozi wa chuo ili kwenda kumuona Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia kufuatilia suala la uanzishaji wa Chuo hiki.

“Mkoa utapambana, kuhakikisha ya kwamba tunawasemea na tunakipigania hiki Chuo kiweze kuanza kwa haraka ili manufaa yaliyotegemewa kutokana na Chuo hiki yaweze kupatikana kwa haraka” amesema Mheshimiwa Hapi. 

Ameeleza kuwa Chuo hiki kikikamilika kitakuwa kichocheo kikubwa cha kukuza uchumi wa Mkoa wa Mara na wananchi wake na kutoa  mfano wa Jiji la Mwanza ambapo kabla ya kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino, Jiji hilo lilikuwa na uchumi wa kawaida na baada ya kuanza kwa Chuo hicho uchumi wa Mwanza ulipanda sana.

Amewapongeza kwa kufanya kazi ya kuanzisha Chuo na kueleza kuwa kazi hiyo ni ngumu na Chuo kimekaa muda mrefu bila kudahili wanafanzi na kupata viongozi wa Chuo.

Ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kuchangamkia fursa ya uwekezaji katika hosteli za wanafunzi ili kuchangamkia fursa hiyo na kuandaa makazi ya wanachuo watakapokuwa wanaanza masomo.

Miradi ambayo ipo katika Chuo hicho ni pamoja na mradi wa ujenzi wa jengo la uchapishaji (University Printing Press) ambao umefadhiliwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ambao umeshajengwa na jengo hilo litatumika kama jengo la utawala kwa kuanzia; mradi wa ujenzi wa miundombinu ya kufundishia utakaofadhiliwa na Benki ya Dunia wa shilingi 103 ambao unategewa kuanza Oktoba 2021; mradi wa ukarabati wa Sekondari ya Oswald Mwang’ombe utakaofadhiliwa na Serikali ya Tanzania kwa gharama ya shilingi bilioni 2.5 na mradi Serikali ya Poland wenye gharama ya shilingi bilioni 183 ambao andiko lake limeshawasilishwa.

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof. Lesakit S. B. Mellau ameeleza kuwa Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Kilimo na Teknolojia kilianzishwa mwaka 2010 kilikuwa kinaitwa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Butiama yaani Butiama University of Agriculture and Allied Sciences lakini baadaye jina la chuo lilibadilika kuakisi nia ya kuanzisha Chuo cha kilimo kwa lengo la kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

“Ili kutekeleza adhma hiyo Serikali ya Mkoa wa Mara Mwaka 2013 kupitia Kamati ya Ushauri wa Mkoa (RCC) iliamua kuwa Chuo Kikuu kijengwe Mkoa wa Mara na kutoa maeneo ya kutosha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo hiki” alisema Prof. Mellau.  

Prof. Mellau ameeleza kuwa Mkoa uliamua kuwa eneo lililokuwa la Kituo cha Uhimilishaji wa Mifugo cha Butiama yaani Butiama Artificial Insemination Center (BAIC) lenye ukubwa wa ekari 573.5 ambalo awali lilijengwa na Cuba kutokana na urafiki wa Hayati Fidel Castro na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kukabidhiwa Wizara ya Kilimo.

Ameyataja maeneo mengine kuwa ni Ikolokonyo lenye ukubwa wa ekari 179 na eneo la Nyambaghembe lenye ukubwa wa ekari 760 katika wilaya ya Butiama; eneo la Kinesi katika Wilaya ya Rorya lenye ukubwa wa ekari 95; na eneo la Kisangula katika Wilaya ya Serengeti lenye ukubwa wa ekari 136; katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere iliyopo katika Manispaa ya Musoma kuna makubaliano ambayo yanaendelea kuzungumzwa kuwa Chuo kitapewa eneo la kujenga chuo ndani ya eneo la hospitali hiyo kwa ajili ya program za afya.

Prof. Mellau ameeleza kuwa wakati Chuo hicho kinaanza aliyekuwa Mbunge wa Butiama Mheshimiwa Nimrod Mkono alijitolea iliyokuwa Sekondari yake ya Oswald Mwang’ombe kuwa Kampasi anzilishi ya chuo hicho.  

Kwa mujibu wa Prof. Mellau mpaka sasa Chuo hicho hakina usajiri wa kudumu na viongozi wa chuo hawajateuliwa ikiwemo Mkuu wa Chuo, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo, Makamu Mkuu wa Chuo, Baraza la Chuo pamoja na kamati nyingine za Baraza la Chuo na kwa sasa Chuo kinaendeshwa na Kamati ya Menejimenti ya Chuo pekeyake kikiongozwa na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma (DVC A) ambaye pia ni Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo. 

 Ameeleza kuwa kutokana na hali hiyo Chuo hiki hakiruhusiwa na Kamisheni ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) kudahili wanafunzi, kazi kubwa wanayoifanya kwa sasa ni kutunga hati idhini, miongozo, mitaala na sheria za uendeshaji wa chuo hicho.

Aidha kwa upande wa watumishi ameeleza kuwa Chuo kinawatumishi 79 na kati yao watatu ni wa ngazi za uprofesa wakati wahadhiri wengine wote waliobakia wapo katika ngazi ya Wahadhiri Wasaidizi.  

Ameuomba Mkoa ardhi zaidi kwa ajili ya upanuzi wa Chuo hicho kutokana na mahitaji ya ardhi kwa Chuo cha kilimo ni kubwa zaidi lakini ardhi iliyopo kwa sasa inaweza isitoshe kwa siku za usoni.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa