• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara kuongeza kasi kugawa vitambulisho vya wajasiriamali

Posted on: May 27th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri mbalimbali Mkoani Mara kusimamia kikamilifu zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali mkoani humo.

Akizungumza katika kikao cha kugawa awamu ya pili ya vitambulisho vya wajasiriamali kwa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa amewataka viongozi hao kuhakikisha kuwa Mkoa unakuwa na ugawaji wa vitambulisho wa asilimia zaidi ya tisini.

“Sasa kila wilaya ya kila Halmashauri ihakikishe kuwa inagawa vitambulisho kwa zaidi ya asilimia 90 hadi mwisho wa zoezi hili, na atakayeshindwa atajieleza kwa nini imeshindikana” alisema Malima.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa katika awamu ya kwanza kwa mwaka huu wa 2020, Mkoa ulifanikiwa kugawa wastani wa asilimia 62 ya vitambulisho vyote na kuwa Mkoa wa 21 kati ya mikoa 26 ya Tanzania Bara.

Mheshimiwa Malima alieleza kuwa hali hiyoilitokana na baadhi ya halmashauri kufanya vibaya sana na kupata chini ya asilimia 50 katika zoezi hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Butiama Mheshimiwa Anarose Nyamubi ameeleza kuwa zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya wafanyabiashara lifanywe na idara zote katika Halmashauri ili kuleta ufanisi zaidi.

Mheshimiwa Nyamubi ameeleza kuwa kila idara inafanyakazi na watu ambapo baadhi yao ni wafanyabiashara ambao wanahitaji vitambulisho vya wajasiriamali.

“Watendaji wa halmashauri nyingi hawakulipokea suala la vitambulisho vya wajasiriamali vizuri na wamekuwa hawana mwamko wa kulifanyia kazi kama inavyotakiwa” alisema Mheshimiwa Nyamubi.   

Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mara Bwana Wallace Mnkando ameeleza kuwa katika awamu hii, vitambulisho vimeletwa kwa namba kwa kutumia mfumo maalum ambao utaiwezesha serikali kufuatilia zoezi la kugawa vitambulisho hivi katika kila hatua.

“Serikali kwa wakati wowote itakuwa na uwezo wa kufuatilia vitambulisho hivi sehemu vilipokwama hatua kwa hatua” alisema Bwana Mnkando.

Katika awamu hii ya pili Mkoa wa Mara umepata vitambulisho 6,000 vitakavyogawiwa katika wilaya za Rorya, Tarime, Musoma, Butiama, Serengeti na Bunda katika Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa