• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara kuanzisha daftari la wahandisi katika miradi ya ujenzi

Posted on: July 12th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kuanzisha daftari maalum la wataalamu wa Uhandisi litakalowekwa katika miradi yote ya ujenzi na ukarabati katika Halmashauri zao ili kurahisisha uwajibikaji wa wahandisi katika utekelezaji wa miradi.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 12 Julai, 2022 kwa nyakati tofauti wakati akihudhuria vikao vya mabaraza ya madiwani katika Halmashauri za Wilaya ya Musoma na Manispaa ya Musoma.

“Ninataka kuwepo na madaftari maalum ambayo wahandisi watayatumia kutoa maelekezo kwa mafundi na wasimamizi wengine wa miradi na kutoa maoni yao ili kurahisisha uwajibikaji wa wahandisi katika miradi ya maendeleo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa amebaini katika baadhi ya miradi ya ujenzi wahandisi hawaitembelei mpaka viongozi wanapoenda kuitembelea na baada ya hapo hawarudi tena kurekebisha mapungufu waliyoelekezwa kuyarekebisha.

“Sasa tunataka mhandisi aidhinishe kila hatua ya mradi kwa maandishi na atoe maelekezo yake yote kuhusiana na mradi kwa maandishi ili kiongozi yoyote akifika katika mradi huo aweze kuyaona ili kuimarisha usimamizi wa miradi ya maendeleo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakuu wa Wilaya na Madiwani kuhakikisha kuwa wahandisi wanasimamia miradi ya ujenzi kwa kukagua madaftari ya miradi na kuchukua hatua kwa wahandisi kwa kukwamisha miradi au hasara itakayotokana na utekelezaji mbovu wa mradi husika.

Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa anaamini madaftari hayo yakisimamiwa vizuri yataimarisha uwajibikaji wa wahandisi, kuboresha usimamizi wa miradi na kupunguza hoja za CAG na mbio za Mwenge wa Uhuru.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kuanzia sasa, kila atakapotembelea mradi atataka kuona madaftari hayo pamoja na maoni au maelekezo yaliyotolewa na wahandisi katika usimamizi wa miradi ya ujenzi na ukarabati katika Mkoa wa Mara.

Maagizo hayo yametolewa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kutembelea Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kuhudhuria vikao vya mabaraza ya madiwani kwa ajili ya kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iliyoanza leo.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa