• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara kuanza kampeni ya matone ya Vitamin A

Posted on: May 31st, 2023

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Khalfani Haule leo tarehe 31 Mei, 2023 amefungua kikao cha Afya ya Msingi (PHC) na maandalizi ya mwezi wa Afya na Lishe ya Mtoto katika Mkoa wa Mara katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Haule ameeleza kuwa katika utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa mwaka jana Mkoa wa Mara haukufanya  vizuri na sehemu moja wapo ni kiashiria cha utoaji wa matone ya vitamin A na ameshukuru sana uwepo wa wafadhili na mashirika yasiyo ya kiserikali katika eneo hili.  

“Ninawataka Wakuu wa Wilaya wote kusimamia vizuri zoezi hili na kuzindua zoezi la utoaji wa matone ya Vitamin A katika maeneo yenu na kuwahusisha viongozi wa maeneo husika wote katika kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa” amesema Dkt. Haule.

Mheshimiwa Haule ameeleza kuwa utoaji wa matone ya vitamin A ambayo ni muhimu sana katika kinga ya mwili, kuzuia upofu na magonjwa mengine.

Aidha, Dkt. Haule amezitaka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kutoa kipaumbele cha kuboresha afya ya watoto kwa kusimamia na kutekeleza kikamilifu mkataba wa lishe.  

Mwakilishi huyo wa Mkuu wa Mkoa ameishukuru Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kuendelea kutoa wataalamu na wadau wote wa afya waliohusika na masuala ya lishe na utoaji wa matone ya Vitamin A kwa kufadhili kikao hicho.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Dkt. Zabron Masatu ameeleza kuwa mpango wa Mkoa wa Mara kwa mwaka huu ni kuwa kinara katika utekelezaji wa Mkataba wa Lishe.

Dkt. Masatu ameeleza kuwa utoaji wa chanjo ya matone ya vitamin A kwa watoto chini ya miaka mitano upo katika viashiria muhimu vya utekelezaji wa mkataba wa lishe hapa nchini.

“Mkoa wa Mara unatarajia kuanza kampeni ya utoaji wa Vitamin A kuanzia tarehe 01-30 Juni, 2023 kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano” alisema Dkt. Masatu.  

Dkt. Masatu ameeleza kuwa utoaji wa matone ya Vitamin A hufanyika mara mbili kila mwaka katika miezi ya Juni na Desemba na masuala mbalimbali ikiwemo utoaji wa Vitamin A, utambuzi wa

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Peter Kaswahili  ameeleza kuwa anaamini maandalizi ya usambazaji wa vitamin A na uhamasishaji katika Mkoa wa Mara umeshafanyika ili kuruhusu zoezi hilo kuanza.  

Dkt. Kaswahili amewataka watumishi wa sekta ya afya watakaohusika na zoezi hilo kujaza taarifa inavyotakiwa katika mfumo ili kuweza kuboresha takwimu za masuala ya lishe katika Mkoa wa Mara.  

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Helen Keller International Dkt. Deogratius Damas Ngome ameeleza kuwa shirika hilo limejikita katika magonjwa ya macho, masuala ya lishe na magonjwa ambayo hayapewi kipaumbele.

Dkt. Ngome ameeleza kuwa Mkoa wa Mara ni miungoni mwa mikoa 14 ambayo ilikuwa haina msaada wa wadau katika kutoa matone ya vitamin A; Mkoa una wakazi wengi kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2022 na kutokana na mahusiano yaliyopo anaamini wanaweza kufanya kazi vizuri zaidi wakiwa katika Mkoa wa Mara.  

 Kikao cha Afya ya Msingi cha maandalizi ya kuanza kwa kampeni ya utoaji wa matone ya vitamin A kimefayika leo tarehe 31 Mei, 2023 katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa