• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara, Arusha zapongezwa Miradi ya GPE Lanes II

Posted on: November 22nd, 2024

Serikali imeipongeza Mikoa ya Mara na Arusha kwa usimamizi na utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo katika sekta ya elimu inayofadhiliwa na mradi wa GPE Lanes II hapa nchini na kuiwezesha Tanzania kuendelea kupata misaada zaidi kutoka kwa wafadhili mbailili ya kuimarisha sekta ya elimu.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha ziara ya siku nne katika mikoa ya Mara na Arusha, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi Dkt. Charles Wilson Mahera amesema miradi yote iliyotembelewa imetekelezwa vizuri na viongozi na wasimamizi wa GPE Lanes II wamefurahishwa na miradi hiyo.

“Miradi yote tuliyoitembelea imetekelezwa kwa kiwango na ubora wa miradi hiyo na wafadhili wamefurahishwa zaidi kuona mchango wa jamii na wanufaika katika utekelezaji wa miradi hiyo” amesema Dkt. Mahera.

Dkt. Mahera amewataka viongozi wa Mikoa na Halmashauri kuendelea kusimamia miradi ya maendeleo kwa viwango na weledi ili kuimarisha miundombinu ya sekta mbalimbali na hususan wakati huu ambapo Serikali imeanza kutekeleza mtaala mpya wa elimu na kutoa fedha za kujenga shule za amali katika mikoa yote hapa nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Msingi na Awali, ambaye katika ziara hiyo amemwakilisha Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Elimu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bibi Susan Nussu amesema ameridhishwa na miradi yote waliyoitembelea na kupongeza kwa namna wasimamizi na watekelezaji wa miradi hiyo walivyojiongeza.

“Katika Shule ya Sekondari ya Ufundi Musoma, wanafunzi wanaosoma ufundi wameshiriki kujenga madarasa na kutengeneza samani jambo ambalo limesaidia shule hiyo kujenga pia ofisi ya walimu kwa kutumia fedha zilizolenga kujenga madarasa mawili na matundu sita ya vyoo” amesema Bibi Nussu.

Bibi Nussu amesema katika Shule ya Msingi ya Ibwagalilo awali watoto walikuwa wanaenda mbali kufuata Shule ya Msingi Nyamalebwe ambayo ndio kwa wakati huo ilikuwa jirani kwa watoto hao na utoro wa wanafunzi katika shule hiyo ulikuwa mkubwa na ufaulu haukuwa mzuri kutokana na umbali huo.

“Kwa sasa ufaulu wa wanafunzi wa Ibwagalilo wanafanya vizuri katika masomo yao na matokeo ya upimaji wa darasa la nne kwa mwaka 2022 na 2023 wamefaulu kwa asilimia 100, utoro hamna na wazazi wameitikia wito wa kuchangia chakula cha wanafunzi” amesema Bibi Nussu.

Bibi Nussu amesema katika Shule ya Msingi ya Ibwagalilo iliyojengwa na wafadhili hao hamna mwanafunzi ambaye hajui kusoma, kuhesabu na kuandika jambo ambalo ni mafanikio baada ya wanafunzi kuboreshewa mazingira ya kujifunzia na kufundishia pamoja na zana za ufundishaji kwa wanafunzi wa awali.  

Viongozi hao wametoa pongezi hizo wakati wa kuhitimisha ziara ya siku nne katika mikoa ya mara na Arusha iliyoongozwa na Balozi wa Sweeden nchini Tanzania Mhe. Charlotta Macias Ozaki pamoja na viongozi wengine wanaosimamia mradi wa Global Partnership for Education (GPE) Lanes II.

Wakiwa katika Mkoa wa Mara wageni hao wametembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Manispaa ya Musoma ambapo wamekatembelea Shule ya Sekondari ya Ufundi Musoma na Shule ya Msingi Mwembeni B.

Katika Wilaya ya Butiama, ugenzi huo umetembelea Shule ya Msingi Bisumwa kukagua ujenzi wa madarasa mawili ya shule ya awali na baadaye kutembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na wakiwa hapo walipokelewa na wanafamilia wakiongozwa na Bwana Makongoro Nyerere.  

Wageni wengine walioshiriki ziara hiyo ni pamoja na Naibu Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Mhe. Olukemi Williams, wasimamizi wa mradi wa GPE Lanes II kutoka Ubalozi wa Sweeden na Uingereza, Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Fedha na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa