• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mapato katika mgodi wa Irasanilo yaongezeka

Posted on: September 13th, 2022

Uzalishaji katika Mgodi wa Dhahabu wa Irasanilo unaomilikiwa na wachimbaji wadogo umeongezeka kwa sasa wanapata wastani wa zaidi ya kilo moja hadi moja na nusu ya dhahabu kwa mwezi jambo ambalo limeongeza ukusanyaji wa kodi na ushuru wa huduma unaotokana na uchimbaji wa madini.

Hayo yameelezwa leo tarehe 7 Septemba, 2022 na Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara Mhandisi Joseph Kumburu wakati akitoa taarifa ya Mgodi huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee na kuongeza kuwa kuongezeka kwa uzalishaji huo kumeenda sambamba na udhibiti wa utoroshaji holela wa madini uliokuwa ukifanyika hapo awali.

“Awali uzalishaji katika Mgodi wa Dhahabu wa Irasanilo ulikuwa chini lakini pia kulikuwa na tatizo la utoroshaji wa madini uliokuwa ukifanyika katika Mgodi Huu” alisema Mhandisi Kumburu.

Mhandisi Kumburu ameeleza kuwa baada ya uzalishaji kuongezeka na kudhibiti utoroshaji wa madini katika mgodi huo, kwa sasa mapato ya Serikali Kuu na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama yameongezeka sana. 

“Mfano ni makusanyo ya ushuru wa huduma (service Levy) kwa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ambapo awali Halmashauri ilikuwa inakusanya shilingi milioni tano kwa mwaka, lakini baada ya maboresho yaliyofanyika kwa sasa Halmashauri inakusanya zaidi ya milioni tano kwa mwezi” alisema Mhandisi Kumburu.

Mhandisi Kumburu ameeleza kuwa ongezeko la ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ni kubwa na hii ni zaidi ya mara kumi ya ushuru wa huduma ambayo mgodi huo ulikuwa unalipa hapo awali kwa mwaka mzima.  

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Butiama Mwal. Moses Kaegele ameeleza kuwa awali Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ilikuwa na mapato kidogo sana yanayotokana na mgodi huo, lakini kwa sasa Mgodi wa Irasanilo umekuwa ni tegemeo la mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.

Amewataka wachimbaji katika mgodi huo kuendelea kulipa kodi na ushuru kwa Serikali ili kuinua huduma za jamii katika eneo la Buhemba na Wilaya ya Butiama kwa ujumla.  

“Tunafahamu kuwa watu wanawarubuni wachimbaji kuacha kutoa kodi na ushuru kwa Serikali, niwaombe tu tuachane kugomea taratibu za kisheria zilizowekwa na Serikali, kwa hilo tutakuwa wakali sana kusimamia mapato ya Serikali” alisema Mheshimiwa Kaegele.

Kwa upande wao, wachimbaji hao pamoja na viongozi wa serikali za vijiji waliokuwepo wameiomba Serikali kuongeza miundombinu ya huduma za jamii ikiwemo shule za msingi na shule za sekondari na Kituo cha Afya.

“Hapa kuna watu wengi sana na kutokana na hilo watoto pia ni wengi sana, shule moja haitoshi zinahitajika shule tatu za msingi na angalau shule mbili za Sekondari katika eneo hili” walisema wachimbaji hao.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Butiama, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara, watumishi mbalimbali kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi afungua kambi ya madaktari bingwa na bobezi 64 Mara

    June 23, 2025
  • Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara wapatiwa mafunzo

    June 20, 2025
  • Mara mshindi wa pili UMITASHUMTA 2025

    June 18, 2025
  • Zingatieni miongozo ya kilimo cha tumbaku- Dkt. Haule

    June 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa