• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Malima: Watanzania tutembelee Serengeti

Posted on: February 23rd, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amewataka watanzania kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ili kujionea urithi mkubwa ambao watanzania tumepewa na mwenyezi Mungu.

Mheshimiwa Malima ameeleza hayo leo tarehe 21 Februari katika eneo la Barafu ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti alipoambatana na wahifadhi wa Serengeti na waandishi wa habari kwa ajili ya kujionea tukio la kuzaliana kwa nyumbu ambalo hutokea katika kipindi hiki kila mwaka.

“Serengeti ni urithi mkubwa sana tuliopewa na Mwenyezi Mungu, na watu kutoka mataifa yote wanakuja kuuangalia lakini sisi wenyenayo hatuji sana kama tunavyotarajiwa” alisema Malima.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa Mkoa wa Mara umejipanga kuhamasisha utalii wa ndani ili kutoa fursa kwa wananchi wake na wawekezaji kuwekeza zaidi katika fursa zinazotokana na utalii wa wanyamapori katika hifadhi hiyo.

Ameeleza kuwa Mkoa unajivunia Serengeti kuwa hifadhi bora ya Afrika kwa mwaka wa pili mfululizo jambo ambalo amesema sio la bahati mbaya bali ni utekelezaji wa mkakati madhubuti wa kukuza utalii hapa nchini.

Amewataka watanzania kuhamasisha uhifadhi endelevu kwa manufaa ya vizazi ya sasa na vizazi vijavyo na kuepukana na ujangili ambao unaua wanyama na kuhalibu ikolojia ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.  

Kwa upande wake Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Bwana Masana Mwishawa ameeleza kuwa nyumbu katika hifadhi hiyo huzaliana kwa siku 28 kila mwaka kati ya miezi ya Februari na Machi.

“Wanyama hawa huzaliana katika kipindi hiki kwa wakati mmoja ni mbinu yao ya ulinzi li kuweza kujilinda na wanyama wanaokula nyama ambao ni wengi katika hifadhi hii” alisema Mwishawa.

Bwana Mwishawa ameeleza kuwa inaadiriwa katika kipindi hiki nyumbu zaidi ya 1,600,000 pamoja na pundamilia na wanyama wengine hukusanyika katika maeneo yenye uwanda wa tambarare ambapo nyumbu takriban 5,000 hadi 8,000 huzaliwa kwa siku na katika msimu mzima nyumbu taktriban 500,000 huzaliwa.  

Bwana Mwishawa ameeleza tukio la kuzaliana kwa nyumbu ni tukio kubwa ambalo ndilo chanzo cha msafara wa nyumbu ambapo baadaye wanavuka mto Grumeti, na baadaye wanavuka mto Mara kwenda hifadhi ya Masai Mara nchini Kenya na baadaye kurudi Tanzania katika tambarare hizo na kuzaliana.

 Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ina eneo la kilomita za mraba 14,800 ambapo asilimia 70 ya eneo lote la hifadhi ya Serengeti lipo katika Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa