• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Malima aipongeza MUWASA kwa kukamilisha miradi kwa wakati

Posted on: March 5th, 2021

MALIMA AIPONGEZA MUWASA KWA UKAMILISHAJI WA MIRADI KWA WAKATI

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameipongeza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Musoma (MUWASA) kwa kukamilisha miradi mikubwa miwili ya maji katika Wilaya ya Serengeti iliyokuwa umekwama kwa muda mrefu.

Mheshimiwa Malima alitoa pongezi hizo wakati alipokagua miradi ya maji miwili inayotekelezwa na MUWASA katika Wilaya ya Serengeti leo tarehe 4 Machi 2021 ambapo ameridhia miradi hiyo kufunguliwa katika maadhimisho ya Wiki ya Maji inayotarajia kuanza tarehe Machi 16 hadi 22 mwaka huu.

“Ninawapongeza sana kwa utekelezaji mzuri wa miradi hii iliyokwama kwa muda mrefu ambayo sasa ipo mbioni kukamilika na kuwapatia huduma ya maji wananchi wa Mji wa Mugumu na baadhi ya vijiji katika Wilaya ya Serengeti”alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima ameitaka MUWASA kujiamini na kuonyesha uwezo wake katika utekelezaji wa miradi ili waweze kupata miradi mingine ya maji ambayo inasuasua katika Mkoa wa Mara ili wananchi wapate huduma ya maji.

Mheshimiwa Malima ametembelea miradi ya ujenzi wa Chujio la Manchira katika mji wa Mugumu na mradi wa ujenzi wa tanki na usambazaji wa maji katika kijiji cha Kitunguruma ambayo awali ilikuwa ikifanywa na wakandarasi wengine na serikali ilisitisha mikataba yao baada ya kushindwa kutekeleza miradi hiyo kwa wakati na kuipa MUWASA kuimalizia kwa kutumia mfumo wa Force Account.    

Aidha Mheshimiwa Malima ameiagiza MUWASA na Meneja wa RUWASA Wilaya ya Serengeti kuangalia uwezekano wa maji ya mradi wa kijiji cha Kitunguruma kusambazwa katika vijiji jirani ili wananchi wengi zaidi waweze kunufaika na miradi hiyo. 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MUWASA Bibi Joyce Msiru ameeleza kuwa mradi wa ujenzi wa Chujio la Manchira ulianza kutekelezwa Machi 2015 na mkandarasi Pet Coorperation Ltd kwa gharama ya shilingi 2,173,513,900 na mkataba huo ulivunjwa tarehe 8 Januari 2020 baada ya mkandarasi kushindwa kukamilisha kwa wakati.

“Baadaye mradi huu tulikabidhiwa MUWASA kwa gharama ya shilingi 947,744,707.40 kuanzia Oktoba 2020 na ulitegemewa kukamilika mwishoni mwa Machi 2021, kwa sasa mradi huu umefikia asilimia 90 ya utekelezaji” alisema Bibi Msiru.

Aidha katika mradi wa kusambaza maji katika Kijiji cha Kitunguruma Bibi Msiru amesema mradi huu ulikuwa unatekelezwa na mkandarasi Urban and Rural Engineering Services Ltd  ya Dar es Salaam kwa gharama ya shilingi 1, 153, 608,780 kuanzia Juni 4, 2018 na ulipangwa kukamilika Juni 4, 2019.

Hata hivyo mkataba huu ulivunjwa na serikali tarehe 2 Desemba 2020 kutokana na kusuasua kwa utekelezaji wa mradi na baadaye serikali ilikabidhi mradi huo kwa MUWASA Mei 2020 na ulitarajiwa kukamilika Desemba 2020.

Bibi Msiru ameeleza kuwa MUWASA wametekeleza mradi huu kwa gharama za shilingi 748,501,193.06 ikijumlisha kiasi ambacho alilipwa mkandarasi wa awali na hivyo serikali kuokoa shilingi 405,107,586.96 na kwa sasa mradi umekamilika kwa asilimia 95 kinachosubiriwa ni TANESCO kufunga transfoma za umeme ili kuanza kusambaza maji katika eneo hilo. 

Kwa mujibu wa Bibi Msiru, miradi hiyo miwili inafadhiliwa na Wizara ya Maji kupitia Mfuko wa Maji.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa