• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Malima aiagiza Serengeti kuwekeza kwenye Kilimo

Posted on: June 15th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameitaka halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kuongeza nguvu katika kilimo ili kupanua uwigo wa mapato ya ndani ya halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Malima ametoa kauli hiyo wakati alipohudhuria kikao maalum cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali kwa mwaka wa fedha 2018/2020.

“Halmashauri hii inauwezo mkubwa wa kuongeza mapato ya ndani kama itatoa kipaumbele katika kilimo cha mazao ya pamba, kahawa, miwa na mazao mengine” alisema Mheshimiwa Malima.

Alisema halmashauri hiyo ina maeneo mazuri na makubwa sana kwa kilimo cha mazao ya chakula na biashara lakini kilimo hakijajapewa kipaumbele katika uwekezaji na ufuatiliaji.

Mheshimiwa Malima alisema kuwa maeneo mengine yanayohitaji kipaumbele katika halmashauri hiyo ni pamoja na mifugo na misitu.

“Bahati nzuri halmashauri hii imebarikiwa vitu viti sana, mapato yake yalitakwa kuwa makubwa sana ukilinganisha na hali halisi iliyopo sasa” alisema Mheshimiwa Malima.

Kwa mujibu wa Mheshimiwa Malima kutegemea mapato yanayotokana na uwepo wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti pekee hakuwezi kuiinua halmashauri hiyo na wananchi wake wote kiuchumi.

Aidha amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji kuweza kuingia katika halmashauri hiyo. Akatolea mfano wa mwekezaji ambaye amejenga hoteli ya kisasa ambaye anaambiwa abomoe kwa sababu eneo hilo linataka kufanyiwa uwekezaji mwingine.

Wakati huo huo katika kikao hicho aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kisangula kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mheshimiwa Samson Riyoba ametangaza kukihama chama hicho na kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM).

Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti katika ukaguzi wa mwaka wa fedha 2018/2019 ilipata hati safi na ilikuwa na hoja za nyuma 37 na hoja mpya 27.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa