• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Makungu: Wakuu wa Shule timizeni wajibu wenu

Posted on: February 18th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo tarehe 16 Februari, 2024 amekutana na kufanya kikao na Wakuu wa Shule za Sekondari za Mkoa wa Mara katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Ufundi Musoma na kuwataka kutimiza wajibu wao kwa maendeleo ya Taifa.

Akizungumza katika mkutano huo, Bwana Makungu amesema Wakuu wa Shule kutokana na majukumu yao wananafasi kubwa sana katika maendeleo ya Taifa letu ikiwa ni pamoja na malezi kwa vijana ili kupata Taifa lenye vijana wenye maadili na nidhamu.

“Mnanafasi ya kutengeneza watu wenye uwezo wa kuwaandaa Watanzania kutoa mchango timilifu katika maendeleo ya nchi yao” amesema Bwana Makungu na kongeza kuwa hayo yote yatafanyika ikiwa watatimiza wajibu wao wa malezi, usimamizi wa ufundishaji na nidhamu katika shule hizo.

Aidha, amewataka kuacha kufanyakazi kwa mazoea na kuanzisha makundi yasiyo na tija baina ya walimu na wanafunzi kwani kazi hiyo sio ya kupigiwa kura, ni kazi ya kuteuliwa kutokana na sifa na hivyo wasivunje taratibu kutoa nafasi ya kupendwa na wasiofuata utaratibu.

Bwana Makungu amewataka Wakuu wa Shule wanapokabiliana na changamoto katika usimamizi wa miradi ya maendeleo katika shule zao watoe taarifa na kuomba ushauri kwa wakuu wa shule wengine, viongozi wa Halmashauri, Mkoa hadi Wizara ili kufanikisha malengo ya Serikali katika utekelezaji wa miradi hiyo.    

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara amewataka Wakuu wa Shule kusimamia ufundishaji wa wanafunzi ili kuwanusuru wanafunzi kusoma kwa miaka  minne na kufeli jambo ambalo linamfanya mwanafunzi huyo asiweze kupata fursa zaidi za kujiendeleza au kuajiriwa kwa baadaye.

Amewataka kusimamia nidhamu na kudhibiti mahusiano yasiyo faa baina ya walimu na wanafunzi na baina ya wanafunzi ili wanafunzi waweze kuzingatia masomo yao na kufaulu mitihani yao.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bwana Makwasa Bulenga amemshukuru Katibu Tawala wa Mkoa kwa kutenga muda na kuzungumza na Wakuu wa Shule ambao ni wadau muhimu katika  usimamizi wa Elimu ya Sekondari.

Bwana Makwasa ameeleza kuwa anategemea mabadiliko makubwa baada ya kikao hicho katika usimamizi na uendeshaji wa shule za Sekondari katika Mkoa wa Mara.

Bwana Makwasa amewashukuru walimu pamoja na changamoto zilizopo katika shule zao wamekuwa wakitafuta ufumbuzi hususan katika kupata walimu wa kujitolea na kutoa taarifa ya upungufu au uchakavu wa miundombinu katika Halmashauri zao.

Kikao hicho kilihudhuliwa pia na Katibu Tawala Wilaya ya Musoma, baadhi ya watendaji wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Maafisa Elimu wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa