• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Makungu ahimiza wafanyakazi kutoa ushirikiano

Posted on: August 5th, 2022

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo tarehe 5 Agosti, 2022 amewasili na kukabidhiwa ofisi na baadaye kuzungumza na Wakuu wa Vitengo na Idara pamoja na wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara katika Ukumbi wa Uwekezaji.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na Wakuu wa Vitengo na Idara na wafanyakazi wakati wa makabidhiano hayo, Bwana Msalika amewahimiza wafanyakazi kutoa ushirikiano baina yao na kati yao na viongozi katika utekelezaji wa majukumu.

“Ninaomba tuendelee na ushirikiano uliopo na ili tutekeleze majukumu yaliyo mbele yetu kwa ufanisi katika kuzisimamia Halmashauri za Mkoa wa Mara” alisema Bwana Msalika.

Bwana Msalika ameeleza kuwa kwa sasa kipaumbele cha Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ni kuongeza makusanyo ya ndani ya Halmashauri na kuwataka wafanyakazi kusimamia kwa weledi makusanyo ya Halmashauri.

Aidha, Bwana Msalika amewataka wafanyakazi kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

Kwa upande wake, aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela amewashukuru wafanyakazi wa Mkoa wa Mara kwa ushirikiano wao katika kutekeleza majukumu.

“Ninawashukuru sana kwa ushirikiano mlionionyesha wakati wote nilipokuwa hapa, ninawaomba muendelee na ushirikiano huo kwa Katibu Tawala mpya ili aweze kutekeleza majukumu yake kwa urahisi zaidi” alisema Bwana Msovela

Katika tukio hilo, Bwana Msovela alimkabidhi ofisi Bwana Msalika tukio ambalo lilitanguliwa na kikao cha Katibu Tawala na Wakuu wa Idara na Vitengo na baadaye kikao na wafanyakazi wote wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Aidha, katika tukio hilo wafanyakazi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa ametoa zawadi kwa Bwana Msovela na wamemkaribisha Bwana Msalika ambaye amewasili leo.

Bwana Msalika aliteuliwa na Rais tarehe 28 Julai, 2022 kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara ambaye anachukua nafasi ya Bwana Albert Gabriel Msovela ambaye amehamishiwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa