• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Majaliwa aweka jiwe la msingi ofisi ya DC Butiama

Posted on: February 28th, 2024

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa leo ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama iliyopo katika Kijiji cha Butiama kwenye eneo lenye ofisi za Serikali.

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi, Mhe. Majaliwa amepongeza mradi huo na kuahidi kuwa Serikali itaendelea kuleta fedha katika Wilaya ya Butiama kwa sababu ni wilaya mpya na nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mhe. Majaliwa ameitaka TBA kukamilisha mradi huo kwa haraka ili kuboresha mazingira ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama na pia aweze kuhamia katika eneo hilo lenye ofisi nyingine zote za Serikali.  

Wakati huo huo, Mhe. Waziri Mkuu amempongeza Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Jumanne Sagini kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya katika jimbo hilo.

Akizungumza wakati wa kuwasalimia wananchi wa Wilaya ya Butiama Mhe. Waziri Mkuu amewashukuru wananchi na viongozi wa Wilaya ya Butiama kwa mapokezi mazuri.

Akitoa taarifa za mradi huo, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Miundombinu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhandisi Richard Moshi ameelza kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara ilitenga fedha kwa ajili ya mradi huo kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 na huendelea kutenga fedha kila mwaka kwa ajili ya ujenzi huo.

Eng. Moshi ameeleza kuwa mradi huo umeanza kutekelezwa tarehe 5 Agosti, 2022 na Mkandarasi wa mradi huo ni Wakala ya Majengo (TBA) kwa gharama ya shilingi 2,041,935,338.32 na muda wa mradi ulikuwa ni miezi 12 hata hivyo muda wa utekelezaji wa mradi huo uliongezwa.

Utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 60 na mpaka wakati huu mkandarasi ameshalipwa shilingi 843,394,728.35 ikiwa ni malipo ya awali na hati za malipo ya pili na ya tatu huku hati ya nne ikiwa imetumwa Hazina kwa ajili ya malipo.

Mhandisi Moshi ameeleza kuwa mradi huo una changamoto ya kasi ndogo ya mkandarasi katika utekelezaji wa mradi inayosababishwa na uwezo mdogo wa kifedha wa mkandarasi hivyo kushindwa kufuata mpangokazi uliowekwa.  

Kwa upande wake, Mhe. Sagini amesema yapo mambo mengi yamefanyika katika Wilaya ya Butiama katika miradi ya maendeleo katika sekta za afya, elimu, Chuo Kikuu cha Butiama na Chuo cha VETA kilichojengwa katika jimbo la Butiama.  

Mhe. Sagini amesema ukarabati wa majengo ya awali ya Chuo kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere Butiama ukarabati umekamilika, wanafunzi wameanza masomo kwa mwaka huu wa masomo na serikali kupitia mradi wa maendeleo ya Vyuo Vikuu unaofadhiliwa na benki ya Dunia imetoa zaidi ya bilioni 100 na kwa sasa ujenzi umeanza.

Akiwa Butiama, Mhe. Majaliwa pia amefanya kikao na watumishi na madiwani, ametembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kupokelewa na wanafamilia, amewasalimia wananchi na kuendelea na ziara yake Wilaya ya Serengeti.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa