• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Magufuli atoa bilioni 33.9 kulipa fidia Nyamongo

Posted on: May 26th, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa John Pombe Magufuli ameidhinisha shilingi bilioni 33.9 kwa ajili ya kulipa fidia kwa wakazi 1,639 wa vijiji viwili vinavyouzunguka Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara katika Wilaya ya Tarime, Mkoa wa Mara.

Malipo ya fidia hizo yameanza kulipwa leo tarehe 20 Mei 2020 kama ilivyoahidiwa awali na Mkuu wa Mkoa wa Mara na kuzinduliwa rasmi na Waziri wa Madini Mheshimiwa Dotto Biteko.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa malipo ya fidia kwa wananchi hao, Mheshimiwa Biteko ameeleza kuwa tarehe 7 Septemba 2018 Rais alipotembelea Nyamongo aliagiza serikali kutatua kero mbili za wananchi wa Nyamongo ambazo ni malipo ya fidia na kudhibiti uchafuzi wa mazingira katika eneo hilo.

“Leo nimekuja hapa kuwaeleza kuwa kero hizi zote mbili serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Magufuli imezitatua” alisema Mheshimiwa Bitteko.

Aidha ameeleza kuwa kwa sasa serikali imekuwa ikifaidika sana na mauzo ya madini kupitia masoko ya madini yaliyopo hapa nchini. Akitolea mfano wa eneo la Nyamongo Mheshimiwa Biteko ameeleza kuwa awali kabla ya kufungua soko la madini serikali ilikuwa inapata fedha kidogo sana lakini kwa sasa mapato yameongezeka maradufu.  

Akizungumza wakati akiwakaribisha waheshimiwa mawaziri kuzungumza na wananchi, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameeleza kuwa malipo haya ni utatuzi wa kero ya muda mrefu sana ya wananchi wa Nyamongo.  

“Suala la kulipa fidia kwa wananchi hawa ni katika matatizo sugu na lilikuwepo kwa zaidi ya miaka 11 mpaka sasa” alisema Malima.  

Mheshimiwa Malima alisema anashukuru ushirikiano ulioonyeshwa na Wizara ya Madini pamoja na Wizara ya Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Mgodi wa Barrick North Mara katika kutatua kero hiyo ya muda mrefu.

Kwa upande wake Diwani wa Nyamongo Mheshimiwa Rashid Bongomba ameeleza kuwa awali wananchi walikuwa na matatizo mengi na mgodi hapo  lakini sana mengi yametatuliwa ilibakia hili la fidia tu kwa wananchi.

“Kwa fidia hii, serikali imesaidia wananchi kurudisha imani yao kwa Chama cha Mapinduzi, na ninawahakikishia kuwa  matokeo yake tutayaona” alisema Mheshimiwa Bongomba.

Aidha aliomba viongozi wa serikali kuangalia uwezekano wa kuleta barabara ya lami Nyamongo ili kutatua kero ya usafiri ya muda mrefu kwa wananchi wa eneo hilo.

Uzinduzi wa kulipa fidia kwa wananchi ulihudhuriwa pia na Waziri Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu; Naibu Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Serikali Mheshimiwa Angelina Mabula na viongozi wengine wa chama na serikali.

Wananchi 1639 wa vijiji vya Nyabichune na Matongo katika eneo la Nyamongo wamelipwa fidia zao kupitia katika akaunti zao za benki.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa