• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Magari haya yatumike kuwahudumia wananchi: Mtambi

Posted on: July 12th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 11 Julai, 2024 amekabidhi magari yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa Wakuu wa Wilaya na kuwataka kutumia magari hayo katika kuwahudumia wananchi.

Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano ya magari hayo Mhe. Mtambi amemshukuru Mhe. Rais kwa kuwapatia Wakuu wa Wilaya Magari hayo ambayo yatawasaidia kuwafikia wananchi na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.

“Magari haya yatumike kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi  na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yenu” amesema Mhe. Mtambi.

Aidha, amewataka Wakuu wa Wilaya kuhakikisha magari hayo yanatunzwa na kuwekwa katika hali nzuri ili yadumu na kutoa huduma kwa wananchi kwa muda mrefu.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya ameeleza kuwa katika awamu hii, Wakuu wa Wilaya za Bunda, Serengeti na Rorya ndio wamepewa magariyaliyopangwa katika bajeti ya mwaka 2023/2024.

Bwana Kusaya amesema Wakuu wa Wilaya za Musoma, Tarime na Butiama wanatarajiwa kupatiwa magari katika bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025.

Bwana Kusaya amemuomba Mkuu wa Mkoa kuyazindua na kuyakabidhi magari hayo ili yaanze kutumika katika kuwahudumia wananchi wa wilaya hizo.  

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Dkt. Vincent Mashinji amemshukuru Mhe. Rais kwa kutoa magari hayo na kuondoa changamoto ya magari waliyokuwa nayo katika utekelezaji wa majukumu yao.

Dkt. Mashinji amesema magari hayo yatawasaidia kuwatembelea na kusikiliza kero za wananchi na kukagua miradi ya maendeleo iliyopo katika Wilaya zetu na kuwataka madereva kuyatunza magari hayo ili yaweze kudumu muda mrefu.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa