• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Madaktari Bingwa 45 waanza kutoa huduma Mara

Posted on: December 2nd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo ameongoza mapokezi ya madaktari bingwa 45 katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na kuwataka wananchi kutumia vizuri fursa ya uwepo wa madaktari hao kupata matibabu.

Akizungumza katika mapokezi hayo, Mhe. Mtambi amemshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha madaktari hao kufanya kambi maalum katika Mkoa wa Mara na kutoa huduma za kibingwa kwa wananchi jirani na makazi yao.

“Kambi ya madaktari bingwa imewezekana kuletwa katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali ya awamu ya Sita katika Sekta ya afya ikiwemo kujenga miundombinu na kununua vifaa tiba na dawa” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema awali huduma za madaktari bingwa na wabobezi zimekuwa zikitolewa Mwanza, Dodoma au Dar es Salaam na wananchi walikuwa wakitumia gharama kubwa kusafiri lakini sasa wamepata bahati huduma hii inapatikana katika Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.  

Mhe. Mtambi amesema kwa mwaka huu, hii ni mara ya tatu Madaktari Bingwa wanaweka kambi maalum katika Mkoa wa Mara ambapo katika miezi ya Juni na Novemba, 2024 madaktari bingwa walifika na kutoa huduma katika Hospitali za Halmashauri na Vituo vya Afya vya Kasahunga na Ikizu katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Mhe. Mtambi amesema uwepo wa madaktari hao unawahakikishia madaktari bingwa hao huduma nzuri ya afya ambayo itaboresha uhai wao baada ya kupata matibabu ya kibingwa na kibobezi kutokana kwa madaktari hao.

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka wananchi kuendelea kufika katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere hata baada ya muda wa kambi hiyo kuisha kwa kuwa hospitali hiyo pia inao madaktari bingwa ambao wataendelea kutoa huduma hata baada ya muda wa kambi hii maalum kuisha.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka amewakaribisha madaktari hao katika Wilaya ya Musoma na kuwataka wananchi wa Musoma kujitokeza kwa wingi kupata huduma kwa madaktari hao.

Mhe. Chikoka amewataka wagonjwa waliojitokeza kwa siku ya leo kuwa mabalozi wazuri wa huduma watakazopata katika Hospitali hiyo na kuwahakikishia kuwa huduma za madaktari bingwa katika hospitali hiyo ni endelevu.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Dkt. Zabron Masatu amesema wataalamu wa Afya katika Mkoa wa Mara wamefurahia sana ujio wa madaktari bingwa hao ambao watasaidia kuwajengea uwezo watumishi na kubadilishana uzoefu wa kutibu wagonjwa.

Dkt. Masatu amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Afya kwa kuandaa kambi ya madaktari bingwa maalum kwa ajili ya wananchi wa Mkoa wa Mara kuweza kupata matibabu hospitalini hapo.

Dkt. Masatu amesema Serikali imefanya uwekezaji mkubwa wa vifaa tiba na dawa katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na hivyo ujio wa madaktari hao utaboresha huduma wanazozitoa kwa wananchi.  

Akizungumza katika mapokezi hayo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dkt. Osmund Dyegura amesema katika madaktari hao madaktari bingwa wa magonjwa ya wanawake ni watano, madaktari bingwa wa upasuaji wanne, madaktari bingwa wa watoto wanne, madaktari bingwa wa upasuaji wa mifupa watatu.

Dkt.Dyegura amesema madaktari bingwa wa pua, sikio na koo wawili, madaktari bingwa wa macho wawili, daktari bingwa wa mfumo wa mkojo mmoja, daktari bingwa wa ngozi mmoja, daktari bingwa wa usingizi mmoja, daktari bingwa wa kinywa na meno mmoja na daktari bingwa wa figo na inni.

Dkt. Dyegura amesema historia ya kambi za matibabu za madaktari bingwa katika Hospitali za Rufaa zilianza mwaka juzi ambapo ilifanyika katika Mkoa wa Simuyu na baadaye ikaendelea katika mikoa mingine na kwa sasa ipo Mkoa wa Mara.

Dkt. Dyegura amesema manufaa ya kambi hiyo ni kusogeza hudumaza kibingwa kwa wananchi, kuwajengea uwezo wataalamu wa sekta ya afya katika utoaji wa huduma na kuibua wagonjwa ambao watatibiwa katika Hospitali za Rufaa za Kanda na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Baada ya mapokezi hayo, Mhe. Mtambi amefanya ukaguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na kuzungumza na wagonjwa waliokuja kwa ajili ya kupata huduma za kibingwa kwa madaktari hao na kusikiliza kero za wananchi.

 Hafla ya mapokezi ya madaktari bingwa imehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Wilaya ya Musoma, baadhi ya watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na wagonjwa waliofika kwa ajili ya kupata matibabu.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa