• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Maandalizi ya Sensa Yakamilika

Posted on: August 23rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee ameeleza kuwa maandalizi ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 katika Mkoa wa Mara yamekamilika.

Akizungumza katika matangazo ya moja kwa moja yaliyorushwa kupitia Kituo cha Redio cha Bunda FM leo, Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa tayari Makarani wa Sensa wapo katika maeneo yao ya kazi na wanaendelea na maandalizi ya kuanza zoezi saa sita usiku wa kuamkia kesho tarehe 23 Agosti, 2022.  

“Maandalizi yote muhimu ya Sensa kwa Mkoa wa Mara yamekamilika, na tayari makarani wapo katika vituo na Wasimamizi wa Sensa wanaendelea kupokea changamoto na kuzitatua kwa kadiri zinavyoendelea kutolewa katika maeneo mbalimbali” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu sura ya 351, taarifa zote zitakazotolewa na wananchi kwa karani wa Sensa zitakuwa ni siri na zitatumika kwa madhumuni ya Sensa na makarani wote wamesaini kiapo cha kutunza siri za taarifa zote atakazozikusanya katika zoezi la Sensa.

“Karani yeyote akithibitika kwenda kinyume na kiapo cha kutunza siri, atashtakiwa na kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria hii, hivyo ninaomba kuwahakikisha wananchi kuwa taarifa watakazozitoa kwa karani wa Sensa zipo salama na hivyo niwaombe watoe taarifa sahihi ili Serikali ipate takwimu sahihi” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ambaye aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu, ameeleza kuwa makarani wa sensa wakienda kuhesabu watu wataambatana na viongozi wa serikali ya mtaa au vitongoji wa eneo husika.

Mheshimiwa Mzee amewaomba wananchi wote wa Mkoa wa Mara kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi la mwaka 2022, kutoa taarifa sahihi kwa makarani wa Sensa na wazazi/walezi wa Watoto/watu wenye ulemavu kuhakikisha watu wote wenye ulemavu wanahesabiwa.

 “Hii itaiwezesha Serikali kutambua idadi ya watu wenye ulemavu katika kila eneo, aina ya ulemavu, msaada unaohitajika na namna bora ya kuweza kuwasaidia mmoja mmoja au kama kundi la watu wenye ulemavu” alisema Mheshimiwa Mzee.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa