• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Maandalizi ya NANENANE yamekamilika

Posted on: July 28th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameeleza kuwa maandalizi ya maonyesho ya kilimo ya NANENANE kwa mwaka 2020 yatakayofanyika kitaifa katika viwanja vya Nyakibindi katika Mkoa wa Simuyu yamekamilika.

Mheshimiwa Malima ameeleza hayo leo tarehe 25 Julai 2020 katika kikao cha pamoja kati ya maafisa wa serikali wa mikoa ya Kanda ya Ziwa Mashariki na wadau wa maonyesho hayo kilichofanyika katika viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.  

“Mpaka sasa sehemu kubwa ya maandalizi haya yapo vizuri na tunaendelea kukamilisha shughuli ndogondogo zilizobakia na tunatarajia tarehe 30 Julai 2020 maonyesho haya yataanza hapa Nyakabindi” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima ambaye kwenye kikao hicho alikuwa Kaimu Mwenyekiti amemtaka Katibu Tawala Msaidizi, Miundombinu wa Mkoa wa Simiyu kuhakikisha anakamilisha shughuli za kuleta huduma za maji, umeme na barabara kabla ya tarehe 29 Julai 2020.

Aidha ameelezea matarajio yake kuwa Waziri wa Kilimo ataongeza mwaka mmoja zaidi kwa Kanda ya Ziwa kuendelea kuandaa maonyesho haya katika uwanja huu wa Nyakabindi.

Aidha amewakaribisha wadau wote wa maonyesho kuja kuanzia tarehe 30 Julai 2020 ili kujionea na kujifunza shughuli mbalimbali za kilimo, mifugo na uvuvi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Zainab R. Telak ameeleza kuwa kazi ya maandalizi ya nanenane iliyofanyika mpaka sasa ni nzuri sana.  

“Kutokana na janga la Corona tulikuwa na wasiwasi lakini kila kitu kimeenda sawa na wadau wengi sana wanashiriki mwaka huu” alisema Mheshimiwa Telak.

Ameeleza kuwa tayari vipando vipo katika hali nzuri na mabanda yanaendelea kujengwa na michango ya wadau inaendelea kupokelewa hivyo bado tu kuyafungua rasmi ili wananchi waweze kupata huduma uwanjani hapo.  

Maonyesho ya Nanenane kwa mwaka 2020 yanafanyika katika uwanja wa Nyakabindi Mkoani Simiyu na yanatarajiwa kuanza tarehe 30 Julai 2020 lakini ufunguzi rasmi utafanywa tarehe 1 Agosti 2020.

Waandaaji wakuu wa maonyesho haya ni mikoa inayounda Kanda ya Ziwa, Mashariki ambayo ni Simiyu, Mara na Shinyanga.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa