• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Maandalizi ya Kushiriki GLITE 2020 yanaendelea vizuri

Posted on: February 20th, 2020

Maandalizi ya Mkoa wa Mara kushiriki katika Maonyesho ya Kimataifa ya Utalii ya “Great Lakes International Tourism Expo” (GLITE) 2020 yanayotarajiwa kufanyika katika uwanja wa CCM Kirumba, Mkoani Mwanza kuanzia tarehe 19 Juni 2020 hadi tarehe 21 Juni 2020 yanaendelea vizuri.

Akizungumza katika kikao cha pili cha wadau wa utalii wa Mkoa wa Mara kilichofanyika tarehe 17 Februari 2020 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Adam Kighoma Malima amesema Mkoa umejipanga kuonyesha vivutio vyake vya utalii, fursa za uwekezaji na kuvitangaza vivutio vipya vya utalii ambavyo havijajulikana bado.

“Sisi katika Mkoa wa Mara tunavivutio vingi sana ambavyo havijajulikana bado na havijatangazwa kabisa”. Alitoa mfano wa eneo la Nduta ambalo limo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambalo nyumbu hulitumia kuzaliana kila mwaka kati ya tarehe 5 hadi 30 Februari. Katika kipindi hiki nyumba takriban 500,000 huzaliwa katika eneo la Nduta.

Mheshimiwa Malima alisema lengo kubwa la kikao hiki cha pili ni kupata mrejesho kutoka kwa Wakurugenzi wa Manispaa, Miji na Wilaya kuhusu vivutio vya utalii vilivyopo katika maeneo yao na fursa za uwekezaji katika vivutio vya utalii.

Akizungumza wakati akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kufungua kikao hicho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bibi. Karolina Mthapula amesema maonyesho ya GLITE 2020 yanalengo la kuwakutanisha wadau wa sekta ya utalii ili kujadili maendeleo ya utalii na kutangaza vivutio vya utalii Kanda ya Ziwa.

Bibi Mthapula amesema Mkoa wa Mara utatumia fursa ya maonyesho haya kutangaza vivutio vya utalii vilivyoko katika mkoa huu.

Mikoa itakayoshiriki katika maonyesho ya GLITE 2020 ni mikoa yote ya Kanda ya Ziwa yaani Mara, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Kagera, Geita pamoja na mikoa ya Tabora na Kigoma.

Kikao cha kwanza cha wadau wa utalii Mkoa wa Mara kilifanyika tarehe 28 Januari 2020 katika ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa