• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi yafana

Posted on: December 19th, 2023

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani katika Mkoa wa Mara yamefanyika leo Desemba 1, 2023 katika eneo la Kisorya, Wilaya ya Bunda huku kauli mbiu ikiwa Jamii Iongoze Kutokomeza UKIMWI.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bunda Dkt. Vincent Anney amesema siku hii ni maalum kwa ajili ya kukumbushana kuwa UKIMWI bado upo tuchukue tahadhari.

Dkt. Anney ameeleza kuwa kwa sasa zana za kupambana na UKIMWI zipo na zinapatikana katika maeneo mengi mijini na vijijini na kwa sasa vipimo ili kujua hali ya afya vinatolewa bure.

Amezitaja Halmashauri zenye maambukizi makubwa kuwa ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma 3.8; Halmashauri ya Wilaya ya Rorya 3.6 na wastani wa Mkoa wa Mara kuwa ni 2.1.

Mhe. Dkt. Anney ameeleza kuwa kila mmoja akitimiza wajibu wake, maambukizi ya UKIMWI yatapungua na hata kuisha kabisha.

Amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa Kamati za Ukimwi za Kata, Vijiji  na ngazi ya Halmashauri zinafanyika na mihutasari ya vikao hivyo inawasilishwa kwenye mamlaka husika ili kupata taarifa ya masuala yaliyojiri katika vikao hivyo.

Amewashukuru wadau mbalimbali ambao wamejitoa kuusaidia Mkoa wa Mara katika mapambano dhidi ya UKIMWI kwa kuimarisha utoaji wa huduma, vifaa tiba na miundombinu ya sekta ya afya.  

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Dkt. Omari Gamuya ameeleza kuwa kwa sasa Mkoa una watu 66,436 wanaoishi na VVU na kati yao 64,315 wanatambua hali yao ya maambukizi .

Dkt. Gamuya ameeleza kuwa kati ya wote wanaojua kuhusu hali zao za maambukizi wanaume ni 20,109 na wanawake ni 44,206 wakati watoto ni 2137 na wakati watu wanaojua hali zao za maambukizi 61,099 wameanza kutumia dawa.

Ameeleza kuwa Mkoa wa Mara una jumla ya vituo vya tiba na mafunzo 174 na vituo vya tohara kinga ya kitabibu kwa wanaume 34.

Kwa mujibu wa Dkt. Gamuya, kwa mwaka 2022/2023 Mkoa wa Mara kwa kushirikiana na wadau umesambaza mipira ya kiume (kondomu) 2,153,740 na kutoa elimu katika maeneo mbalimbali.

 Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yamehudhuriwa na viongozi wa Wilaya ya Bunga, maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Wawakilishi kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara, wadau na wananchi.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa