• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Lusasi: Wakaguzi wa Ndani zingatieni Maadili ya Kitaaluma

Posted on: September 2nd, 2024

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Dominicus Lusasi leo tarehe 30 Agosti, 2024 amefunga mafunzo ya wiki mbili kuhusu mifumo kwa Wakaguzi wa Ndani wa Mkoa wa Mara na kuwataka maafisa hao kuzingatia maadili ya kitaaluma.

Akizungumza katika hafla ya kufunga mafunzo hayo, Bwana Lusasi amewataka Wakaguzi wa Ndani kuzingatia miiko ya Ukaguzi wa Ndani katika utendaji wao ili kuhakikisha fedha za Serikali zinatumika kulingana na madhumuni yake na sio vinginevyo.

“Wakaguzi wa Ndani mna majukumu makubwa sana ambayo mnawajibika nayo kama wanataaluma ikiwemo kuhakikisha taasisi ina taswira nzuri katika jamii kwa kulipa wadeni wake ikiwa ni pamoja na watumishi na wazabuni” amesema Bwana Lusasi.

Amesema, kwa sasa utekelezaji wa shughuli nyingi za Serikali unafanyika katika mifumo hivyo ni vizuri Wakaguzi wa Ndani wakaijua mifumo hiyo vizuri ili kuweza kukagua utekelezaji wa shughuli za Serikali kwa ufasaha na kutoa ushauri mzuri kwa Maafisa Masuhuri wao.

Bwana Lusasi amewataka Wakaguzi wa Ndani kufuatilia mali za taasisi zao zilizoko maeneo mbalimbali na kujiridhisha na usahihi wa mali hizo kuwepo katika maeneo zilipo na kuwashauri Maafisa Masuhuri kuhusiana na taratibu za Serikali.  

Bwana Lusasi amesema Serikali inaleta fedha nyingi sana katika Mikoa na Halmashauri mbalimbali lakini matumizi yake kwa sehemu kubwa sio sahihi na Wakaguzi wa Ndani ni moja kati ya watu ambao wanatakiwa kuijulisha Serikali kuhusu yanayoendelea katika maeneo yao.

“Wewe ndio jicho la taasisi yako, unatakiwa kumshauri Afisa Masuhuri kuhusu yanayoendelea katika ofisi yake kwa ukweli na uwazi, ukiona mambo hayaendi sawa na ukakaa kimya ujue wewe ni sehemu ya tatizo” amesema Bwana Lusasi.

Aidha, amewataka Wakaguzi wa Ndani kufuatilia taratibu za matumizi ya force account kwenye miradi ya maendeleo na manunuzi nje ya mfumo wa NEST na yayoyozingatia taratibu za manunuzi mambo ambayo amesema yakifanyiwa kazi vizuri yanaweza kupunguza hoja nyingi za ukaguzi wanapokuja wakaguzi wa nje.  

Bwana Lusasi ameiomba TAMISEMI kutoa mafunzo zaidi ya mifumo kwa Wakaguzi wa Ndani wa Mikoa na Halmashauri hapa nchini ili kuwajengea uwezo Wakaguzi wa Ndani ikiwa ni pamoja na kuviimarisha Vitengo vya Ukaguzi wa Ndani ili viweze kukagua utekelezaji wa shughuli za Serikali na kuishauri kuhusu mapungufu yaliyomo katika taasisi mbalimbali kwa ufasaha.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Menejimenti, Usimamizi na Ufuatiliaji (MMI) Bwana Marco Maduhu amewashukuru washiriki kwa ushiriki mzuri katika mafunzo hayo, na kuwaahidi kuwa ofisi yake itaendelea kuratibu mafunzo mbalimbali kwa wakaguzi wa ndani kwa kadiri ya mahitaji.

Kwa upande wake, Mhasibu kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bwana Adolph Tikikunda ameushukuru Mkoa wa Mara kwa kuandaa mafunzo hayo kwa Wakaguzi wa Ndani na kuutaka kuendelea kuwajengea uwezo watumishi ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Bwana Tikikunda amewataka Wakaguzi wa Ndani kuendelea kushirikiana kuboresha utendaji wao sehemu za kazi.

Aidha, amesema kwa sasa MMI inaandaa mafunzo ya wiki moja kuhusu ukaguzi wa miradi na mikataba ya ujenzi kwa Wakaguzi wa Ndani ili kuwawezesha kufanya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika maeneo yao.

Bwana Maduhu amewataka Wakaguzi wa Ndani kuboresha utendaji wao na hususan ukaguzi ili kuhakikisha fedha za Serikali zinatumika kwa mujibu wa sheria, taratibu na maelekezo ya Serikali na kwa kuzingatia ubora na muda wa ukamilishaji wa miradi ya maendeleo.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki, Bwana Dismas Shadrack Waguma, Mwenyekiti wa Mafunzo hayo ameipongeza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa kuratibu mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo kuhusu mifumo mbalimbali ya Serikali.

Bwana Waguma ameuomba Mkoa kuendelea kuratibu mafunzo kama hayo mara kwa mara ili Wakaguzi wa Ndani waielewe mifumo mbalimbali ya Serikali na waweze kukagua utekelezaji wa shughuli za Serikali katika mifumo husika.

Bwana Waguma amesema washiriki wametoa maazimio mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuiomba Serikali kukamilisha dirisha la ukaguzi katika Mfumo wa Manunuzi ya Umma (NEST) ili ukaguzi wa manunuzi yanayofanyika ufanyike kwenye mfumo huo.

Aidha, wamependekeza katika mfumo wa GoTHOMIS kuwa sehemu zote za mfumo huo zitumike ili kuweza kupata manufaa halisi ya mfumo huo na Mkoa uwasaidie kuratibu upatikanaji wa nywila za kuingilia katika baadhi ya mifumo ya Serikali.

 Mafunzo hayo ya wiki mbili yaliwahusisha Wakaguzi wa Ndani kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara, Kitengo cha Tehama na baadhi ya maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa