• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

LAAC yapongeza usimamizi wa miradi Tarime TC

Posted on: March 22nd, 2024

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) leo imefanya ziara Halmashauri ya Mji wa Tarime ambapo imeipongeza Halmashauri hiyo kwa usimamizi mzuri wa mradi wa ujenzi wa jengo la utawala na mradi wa ujenzi wa soko la kimkakati la Mji wa Tarime.

Akizungumza katika kikao cha majumuisho, Makamu Mwenyekiti wa LAAC Mhe. Stanslaus Mabula amepongeza ujenzi wa jengo la utawala na usimamizi mzuri wa mradi huo uliopelekea kukamilisha mradi na kubakisha fedha.

“Kazi iliyofanyika hapa kwenye jengo hili ni kubwa sana na mmefanikiwa kujenga uzio kuzunguka ofisi na kibanda cha mlinzi kazi ambazo hazikuwa sehemu ya mradi huu na kubakiza shilingi milioni 82 katika utekelezaji wa mradi huu” amesema Mhe. Mabula.

Hata hivyo, ameitaka Halmashauri hiyo kujibu hoja za ukaguzi zilizoibuliwa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kuhusu malipo ya awali aliyopewa  mkandarasi wa jengo la utawala, Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), shilingi 258,872,578.56.

Mhe. Mabula ameitaka Halmashauri hiyo kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za manunuzi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na amempongeza Mhandisi wa Halmashauri hiyo kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo.

Mhe. Mabula amesema kuwa jengo la Halmashauri hiyo lina ramani nzuri ambazo hazitumiki kwa katika kujenga majengo ya utawala ya Halmashauri ikilinganishwa na jengo la Halmshauri ya Wilaya ya Tarime lenye ramani inayotumika kwa sasa ambayo amesema sio nzuri kama ramani za awali.  

Akizungumzia ujenzi wa soko, Mhe. Mabula ameitaka Halmashauri kuhakikisha inarejesha malipo ya awali aliyopewa mkandarasi wa mradi huo Mohamed Builders shilingi bilioni 1.27 kabla ya mradi haujakamilika na kumtaka Katibu Tawala wa Mkoa kufuatilia utekelezaji wa agizo hilo.  

Akitoa ufafanuzi kuhusu malipo ya mkandarasi wa jengo la utawala, Mhandisi wa Halmashauri hiyo Eng. Daudi Bucheye ameeleza kuwa ni kweli kulikuwa na mapungufu katika malipo ya awali aliyolipwa TBA, hata hivyo baada ya kukaa pamoja na mkandarasi imebainika kuwa katika milioni 500 alizopewa tayari shilingi 374,340,530.25 zimerejeshwa.

“Shilingi 125,659,469.75 bado hazijareshwa kwa malipo ya hati ya nane ya tarehe 22 Septemba, 2023 na Halmashauri bado inayo fedha ya zuio ya shilingi 110,430,456.42 ambayo kama itachukuliwa, mkandarasi bado atakuwa anadaiwa shilingi 15,229,001.33” amesema Mhandisi Bucheye.

Aidha, Mhandisi Bucheye ameieleza Kamati hiyo kuwa Halmashauri imeanza kutumia kanuni mpya ya kumkata mkandarasi anayejenga soko fedha alizopewa awali na kwa kutumia kanuni hiyo mradi utakapofikia asilimia 80 ya malipo, mkandarasi atakuwa ameshakatwa fedha yote aliyolipwa awali ili Halmashauri isibakie na deni.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI Bibi Fortunata Matinde ameeleza kuwa TAMISEMI imepokea maelekezo ya Kamati na itafuatilia utekelezaji wake kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Bibi Matinde ameihakikishia Kamati hiyo kuwa TAMISEMI itahakikisha Halmashauri inazingatia masuala ya kisheria katika utekelezaji miradi mbalimbali kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu.

Ameeleza kuwa suala la mabadiliko ya ramani za majengo ya utawala ya Halmashauri Ofisi ya Rais TAMISEMI italifanyiakazi kwa kuzingatia maoni ya Kamati ili kupata ramani nzuri zaidi zenye ubora katika majengo ya Halmashauri hapa nchini.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya ameihakikishia Kamati hiyo kuwa Mkoa wa Mara umeyapokea maelekezo yote ya Kamati na utasimamia utekelezaji wa maagizo yote kwa wakati.

Bwana Kusaya amesema Mkoa pia utasimamia ukamilishaji wa mradi wa soko la kimkakati la Halmashauri ya Mji wa Tarime kwa ubora na wakati kwa mujibu wa mkataba ili wananchi waanze kupata huduma.  

Ziara hiyo imehudhuriwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, maafisa kutoka TAMISEMI, Ofisi ya Bunge, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na kadhalika.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa