• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kusaya awataka wananchi kushiriki Kampeni ya Msaada wa Kisheria

Posted on: December 10th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya leo amezungumza na Waandishi wa Habari kuhusu uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika Mkoa wa Mara utakaofanyika tarehe 11 Desemba, 2024 katika Uwanja wa Mukendo, Manispaa ya Musoma.

Akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake, Bwana Kusaya amewataka wananchi kushiriki uzinduzi wa kampeni hiyo na katika Kata, Mitaa na Vijji vitakavyofikiwa na kampeni hiyo katika Mkoa wa Mara.

“Hii ni fursa kubwa ambayo Serikali imeileta kwa wananchi kuweza kupata elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kisheria, uraia na utawala bora na huduma zote zitatolewa bure bila malipo yoyote” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amesema Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa Kampeni hiyo katika Mkoa wa Mara atakuwa ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (MB.) na kauli mbiu ya kampeni hii ni “Msaada wa Kisheria kwa Haki, Usawa, Amani na Maendeleo”.

Bwana Kusaya amesema kwa wakati huu, kampeni hii inaendeshwa katika mikoa minne hapa nchini ambayo ni Iringa, Songwe, Mara na Morogoro.

Bwana Kusaya amesema kampeni hii itatekelezwa katika Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara na kuzifikia Kata 10 kwa kila Halmashauri na Mitaa/Vijiji vitatu kwa kila Kata katika kipindi cha siku tisa kuanzia tarehe 11 Desemba, 2024 hadi tarehe 20 Desemba, 2024.

Wakati huo huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya amefungua kikao kazi cha wataalamu kuhusiana na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria kinachoendelea katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na kuwataka wataalamu wanaoshiriki kikao hicho kutoa ushirikiano.

Akizungumza katika kikao kazi hicho, Bwana Kusaya amewataka wataalamu walioshiriki kikao hicho kusikiliza kwa makini na kutoa ushirikiano kwa waandaaji ili kwenda kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Mratibu wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika Mkoa wa Mara Bwana Laurent Burilo amesema katika kampeni hii, wanatarajia kuzifikia Halmashauri zote na Kata 10 na vijiji/ mitaa mitatu katika kila kata.

Bwana Burilo amesema mpaka sasa katika mikoa iliyopita wamehudumia wananchi wengi na changamoto kubwa walizoziona ilikuwa ni uelewa wa masuala ya sheria, migogoro ya ardhi na ukatili wa kijinsia.

“Katika mikoa ambayo tayari imefikiwa na kampeni hii kuna maeneo mengi wanaume wanaofanyiwa ukatili wa kijinsia walijitokeza na kuwasilisha malalamiko yao kwa wataalamu na wakapatiwa msaada wa kisheria” amesema Bwana Burilo.

Bwana Burilo amesema katika kampeni hii pia elimu kuhusu masuala ya Uraia na Utawala Bora itatolewa kwa kushirikiana na wadau.  

Bwana Kusaya amesema kampeni hii ilianza kutekelezwa Mkoa wa Dodoma tarehe 28 Mei, 2023 baada ya kuzinduliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (Mb) tarehe 27 Mei, 2023 Jijini Dodoma na mpaka sasa Kampeni hii imeshafanyika katika mikoa mingine saba.

 Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia inafanyika hapa nchini kwa miaka mitatu kuanzia mwezi Machi, 2023 hadi mwezi Februari, 2026 katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Demokrasia inaendelea kupevuka katika Mkoa wa Mara: Mtambi

    October 16, 2025
  • Biteko aitaka CWT kuendana na kasi ya mabadiliko duniani

    October 16, 2025
  • RC awapokea Maafisa na wanafunzi kutoka Chuo cha Jeshi cha CSC

    October 13, 2025
  • RC awapokea Madaktari Bingwa wa Mama Samia 64 Mara

    October 13, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa