• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kusaya awataka Wakurugenzi kuongeza bajeti ya Ustawi wa Jamii

Posted on: July 22nd, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya leo tarehe 19 Julai, 2024 ameongoza kikao cha tathmini ya Programmu Jumuishi ya MAlezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto na kuwataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuongeza bajeti ya Vitengo vya Ustawi wa Jamii ili viweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Bwana Kusaya amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kutenga magari kwa ajili ya Maafisa Ustawi wa Jamii ili waweze kufuatilia kwa ukaribu changamoto za wananchi na hususan watoto katika maeneo mbalimbali wanayofanyia kazi.

“Tukiviwezesha Vitengo vya Ustawi wa Jamii tutapunguza wananchi wenye kero wanaokuja kuwaona viongozi kwa kero mbalimbali, kwa sababu Maafisa Ustawi wa Jamii watazipunguza baadhi ya kero hizo” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya pia amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha programu hii inazinduliwa katika ngazi za Kata, Mtaa na Vijiji katika Halmashauri zote na kuipongeza Halmashauri ya Mji wa Tarime kwa kufanikiwa kuzindua programu hiyo katika Kata zake zote nane za Halmashauri hiyo.

Bwana Kusaya amesema programu hii inawaleta pamoja wadau wa maendeleo wa sekta mbalimbali ili waweze kufanyakazi kwa ushirikiano katika kuhakikisha watoto wenye umri wa miaka 0-8 wanapata huduma za malezi jumuishi, wanastawi na kufikia hatua za ukuaji timilifu.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara amesema programu hii inatekelezwa katika vipengele vikuu vitano ambavyo ni lishe toshelevu, malezi yenye mwitikio, ulinzi na usalama, afya bora na fursa za ujifunzaji wa awali.

Kwa upande wake, Bibi Mary Shillah Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum ameupongeza Mkoa wa Mara kwa uwakilishi mzuri wa maafisa wa Serikali na wadau wengi kujitokeza katika kikao hicho.  

Bibi Shillah ameeleza kuwa Serikali imeamua kufuatilia watoto katika umri wa miaka 0-8 kwa sababu wataka wadau wengine waongezeke kama vile Benki ambazo zina akaunti maalum za watoto,

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mara Bi. Elizabeth Mahinya amewaomba Wakurugenzi wa Halmashauri kuongeza bajeti ya Vitengo vya Ustawi wa Jamii ili vitengo hivyo viweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi katika kuihudumia jamii.

Bi. Mahinya amesema watendaji waliopo wanaweza kutekeleza majukumu yao vizuri lakini wanakwamishwa na bajeti zinazotengwa katika vitengo hivyo katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Aidha, Bi. Mahinya amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii kufanyakazi kwa ushirikiano ili kwa umoja wao waweze kupata matokeo makubwa katika kuwahudumia wananchi.

Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto ilianza kutekelezwa mwaka 2021/2022- 2025/2026 na ilizinduliwa rasmi tarehe 13 Desemba, 2021 katika Jiji la Dodoma na Mhe. Doroth Gwajima Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum.

 Kikao hicho kimehudhuriwa na Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Maafisa Ustawi wa Jamii na wadau mbalimbali wanaoshirikiana na Halmashauri katika kutekeleza programu hiyo katika Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa