• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kusaya apokea vifaa vya mapambano dhidi ya HIV/UKIMWI

Posted on: May 6th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mara, ndugu Gerald Msabila Kusaya leo Mei 5, 2025 amepokea vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 43.5 kutoka Shirika la Kimataifa lisilo la Kiserikali la AHF ambalo linajihusisha na mkakati wa kufanikisha udhibiti wa HIV na UKIMWI Duniani.

“AHF ni wadau wetu wakubwa katika mapambano dhidi ya HIV na UKIMWI, ninawashukuru kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Mara, Mhe Kanali Evans Mtambi, ninatoa ahadi kuwa tutavitunza vifaa hivi vizuri, vitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa, ninaposhukuru hapa maana yake tunaendelea kuomba tena, kama mkipata tena uwezo huo msisite kutoa msaada zaidi.

Ndugu Kusaya amelishukuru Shirika la AHF kwa msaada huo utakaosaidia wataalamu wa afya kutoa huduma bora kwa wananchi katika mapambano dhidi ya HIV/UKIMWI katika maeneo yao.

Bwana Kusaya amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya za Tarime na Rorya kutunza vifaa hivyo na vifanye kazi iliyokusudiwa ili mabadiliko yaonekane kwa yale malengo ambayo hayajafanikishwa yafanikishwe.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo, Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Dkt. Khalifan Lekizenda, ameeleza kuwa vifaa vilivyopokelewa ni kwa ajili ya Vituo vya Afya vya Utegi na Changuge ni muhimu katika kuboresha huduma kwa wanan.

“Msaada huu ni muhimu ili kuboresha huduma kwa wananchi, mathalani wataalamu watatumia pikipiki kuwatafuta wagonjwa waliotoroka dawa ili waendelee na matibabu na kompyuta zitasaidia katika kuhifadhi taarifa za wagonjwa wakati televisheni itasaidia katika kutoa elimu ya afya na namna ya kujikinga” amesema Dkt. Lekizenda.

Kwa upande wake Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Dkt. Amini Wasomana amesema vifaa vilivyopokelewa ni kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Nyangoto kilichopo katika eneo la Nyamongo.

 “Ninashukuru kwa kupokea msaada wa vifaa hivi na niahidi kwa niaba ya wenzangu vitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa” amesema Dkt. Wasomana.

Kwa upande wake Mratibu wa Huduma za Kudhibiti UKIMWI na magonjwa ya Ngono na homa ya Inni Mkoa wa Mara Dkt.Omari Gamuya amewashukuru wadau kwa vifaa walivyotoa,

“Hivi ni vifaa muhimu kwa VVU na UKIMWI na bado mpaka sasa kwa utafiti wa mwaka wa 2022/2023 Mkoa wa Mara una maambukizi asilimia 5 ambayo ni juu ya hali ya wastani wa maambukizi ya kitaifa.” Amesema Dkt. Gamuya.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Meneja Mkazi wa AHF Tanzania Bi Aika Mtui amesema kuwa shirika lao linafanya kazi kwa miaka karibu 40 sasa dunia nzima.

“Kwa sasa tupo katika nchi 52, tunashirikiana na Wizara ya Afya ya Tanzania kwa magonjwa ya Kifua Kikuu na magonjwa yote ya ngono kwa mikoa miwili ya Mara na Simiyu baada ya kufanya uchambuzi yakinifu ili kuboresha huduma hizo.” Amesema Bi. Mtui.  

Vifaa vilivyopokelewa ni kompyuta za mezani zenye thamani ya shilingi milioni 15,222,000/=, Simu za mkononi za kisasa zenye thamani ya shilingi milioni 2,690,000/=, printa zenye thamani ya shilingi 6,018,000/=, luninga zenye thamani ya shilingi 5,133,000/=, vihifadhia kumbukumbu venye thamani ya shilingi 672,000/=, pikipiki zenye thamani ya shilingi milioni 13,500,000/=.

 Hafla hiyo imehudhuriwa na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Dkt. Zabron Masatu, baadhi ya watumishi kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Halmashauri za Rorya na Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Kusaya apokea vifaa vya mapambano dhidi ya HIV/UKIMWI

    May 06, 2025
  • Mtambi ataka elimu zaidi kutunza Maeneo ya Urithi wa Dunia

    May 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa