• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

Posted on: July 25th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mara Ndugu Gerald Musabila Kusaya leo tarehe 25 Julai, 2025 amepokea jengo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama baada ya Mkandarasi Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kukamilisha ujenzi wa jengo hilo.

Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano ya jengo hilo, Ndugu Kusaya amesema ameridhika na hatua iliyofikia ya ujenzi wa jengo hilo na kwa sasa Mkuu wa Wilaya ya Butiama anaweza kuhamia katika jengo hilo.

“Nimeridhika na ujenzi wa jengo hili, kwa sasa Mkuu wa Wilaya ya Butiama anaweza kuhamia katika jengo hili huku akisubiria samani kwa ajili ya ofisi hiyo ambazo zitanunuliwa hivi karibuni” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amemuagiza Meneja wa TBA Mkoa wa Mara kufanyiakazi marekebisho madogo madogo yaliyobainika katika jengo hilo haraka iwezekanavyo ili Mkuu wa Wilaya atakapohamia jengo liwe vizuri.

Aidha, ameitaka TBA kutoa mafunzo kuhusu mifumo mbalimbali iliyofungwa katika jengo hilo kwa watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama ili waweze kuitumia kwa usahihi mifumo hiyo.

Bwana Kusaya amemtaka Katibu Tawala wa Wilaya kuandaa ulinzi wa jengo hilo baada ya mkandarasi kuondoka katika jengo hilo. 

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Miundombinu Mhandisi Richard Moshi amemshukuru Katibu Tawala wa Mkoa kwa kupokea jengo hilo na kumuomba Mkandarasi kukamilisha marekebisho madogo madogo yaliyobainishwa kabla ya Mkuu wa Wilaya hajahamia katika jengo hilo.

“Haitapendeza Mhe. Mkuu wa Wilaya yupo ofisini harafu fundi anapita kurekebisha vitu katika jengo hili” amesema Mhandisi Moshi.

Kwa upande wake, Meneja wa TBA Mkoa wa Mara Arch. Jeje Nicolaus Jeje amesema marekebisho yote yaliyobainika katika ukaguzi huo yatafanyiwa kazi hadi tarehe 30 Agosti, 2025 yatakuwa yamekamilika.

“Kwa sababu marekebisho ni kidogo, ninaahidi hadi tarehe 30 Agosti, 2025 jengo hili litakuwa tayari kwa ajili ya matumizi ya Mhe. Mkuu wa Wilaya” amesema Arch. Jeje.

Arch. Jeje amesema watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya watapatiwa mafunzo ya namna ya kutumia mifumo mbalimbali iliyofungwa katika jengo la ofisi hiyo mapema iwezekanavyo ili kuwawezesha kuitumia vizuri mifumo hiyo.

Wakati huo huo, Katibu Tawala wa Mkoa ametembelea Wakala wa Umeme na Ufundi (TEMESA) na Gereji ya Jassie zilizopo Manispaa ya Musoma kwa ajili ya kukagua maendeleo ya matengenezo ya magari ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara yanayotengenezwa katika gereji hizo.

 Katika ziara hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa ameambatana na baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Mkoa wa Mara na watumishi wa TBA na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • Mtambi aitaka FEZA kuwekeza Butiama kumuenzi Mwalimu Nyerere

    July 25, 2025
  • Mtambi amtaka mkandarasi mradi wa maji Rorya/Tarime kufanyakazi usiku na mchana

    July 22, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa