• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kituo cha Afya Genkuru kilichotumia milioni 700 hakijakamilika

Posted on: August 16th, 2021

Mradi wa upanuzi wa Zahanati ya Kijiji cha Genkuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime uliotengewa zaidi ya milioni 700 haujakamilika huku fedha zikitumika kununua vifaa vingi vilivyobakia stoo.

Hayo yamebainika leo tarehe 13 Agosti 2021 katika ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mara aliyoifanya katika mradi huo unaojengwa kwa fedha za uwajibikaji kwa jamii zilizotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa North Mara mwaka 2018.

Kufuatia tatizo hilo Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameagiza kukamatwa kwa watu wote waliohusika kwa namna moja au nyingine na mradi huo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

“Nawaagiza Polisi na TAKUKURU kukamata watu wote wanaohusika na mradi huu ili waweze kuzirejesha fedha zilizotumika vibaya katika mradi huu” alisema Mheshimiwa Hapi.

Akikagua mradi huo Mheshimiwa Hapi ameshuhudia vifaa vingi vikiwa vipo stoo na vingine kama vile matofali, karatasi za kuzuia maji, vigae, nondo na mabati vikiwa vimebakia kwa wingi lakini havihitajiki tena.

Mheshimiwa Hapi amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kuchunguza uhalili wa matumizi ya fedha nyingine ambazo zililetwa katika kijiji hicho.

Fedha hizo ni shilingi milioni 100 zinazodaiwa kupelekwa kijiji kingine; milioni 37 zinazodaiwa kulipa mawakili waliosimamia kesi; milioni 15 zinazodaiwa kulipa wadhamini wa kesi; huku milioni 18 zikilipwa viongozi wa kijiji waliokuwa wanahudhuria kesi Mahakama Kuu, Mwanza.

Kwa upande wake Mtendaji wa Kijiji cha Genkuru Bwana Gichovu Chacha  ameeleza kuwa vifaa vilivyonunuliwa vilitokana na maelekezo waliyopewa na Afisa Mununuzi na Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ambao ndio walikuwa wataalamu katika utekelezaji wa mradi huo.

Bwana Chacha ameyataja majengo yaliyojengwa katika mradi huo kuwa ni cliniki ya Baba, Mama na Mtoto (RCH), jengo la Mama na Mtoto, jengo la upasuaji, mochwari, maabara na nyumba moja pacha ya watumishi, choo cha matundu manne.

Mtendaji huyo ameeleza kuwa hamna jengo hata moja lililokamilika baada ya fedha nyingi kutumika kununua vifaa ambavyo havihitajiki tena katika mradi huo huku fedha za kukamilisha mradi huo zikiwa hamna.

 Wakizungumza na Mkuu wa Mkoa wananchi wa kijiji hicho wameeleza kuwa huu ni mwaka wa kumi uongozi wa kijiji chao hauwapi taarifa za mapato na matumizi ya kijiji chao.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa