• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru awapongeza wananchi kwa kujenga shule

Posted on: June 24th, 2021

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Lt. Josephine Paul Mwambashi amewapongeza wanachi wa kijiji cha Balata kwa kujenga shule ya sekondari tarajali ili kupunguza umbali wa wanafunzi kwenda kufuata masomo katika shule iliyokuwa jirani.

Lt. Mwambashi ametoa pongezi hizo wakati wa kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa shule hiyo ambapo madarasa manne na ofisi moja ya walimu yapo katika hatua mbalimbali katika ujenzi wake.

“Ninawapongeza sana wananchi kwa kuona umuhimu wa elimu ya watoto wenu na kuwapunguzia umbali wa kutembea kufuata masomo” alisema Mwambashi.

Lt. Mwambashi ameeleza kuwa kitendo cha wananchi wa Kijiji cha Balata ni mfano wa kuigwa hata na wananchi wa sehemu nyingine ili kuweza kujiletea maendeleo yao kwa haraka.

Hata hivyo mradi huo ulikuwa na mapungufu kadhaa yaliyosababishwa na wataalamu waliokuwa wanausimamia kutokuweka vizuri nyaraka za mradi na kutokupima vifaa vilivyotumika katika ujenzi wa shule hiyo.

“Mwenge unaweka jiwe la msingi lakini naagiza nipate maelezo kutoka kwa Mhandisi kwa nini kupima vifaa ni gharama na vilelezo vya nyaraka zote ambazo hatujapata hapa hadi saa 12 jioni ya leo” alisema Mwambashi.

Katika kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kijiji cha Balata, Mbunge wa Tarime Vijijini Mheshimiwa Mwita Waitara ameahidi kutoa shilingi milioni kumi kutoka katika mfuko wa jimbo ili kuongeza nguvu katika juhudi za wananchi hao.

“Mimi ninawapongeza sana kwa juhudi zenu, mmefanya jambo kubwa sana kwa maendeleo ya watoto wenu na Taifa kwa ujumla, mimi nitawaunga mkono kwa kutoa shilingi milioni 10 kutoka katika mfuko wa jimbo ili ziweze kusaidia” alisema Mheshimiwa Waitara.

Mheshimiwa Waitara ambaye pia ni Naibu Waziri katika Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi aliungana na msafara wa Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Wilaya ya Tarime.      

Aidha mwenge wa uhuru umeweka jiwe la msingi katika barabara ya Kewanja hadi Nyangoto katika eneo la Nyamongo yenye urefu wa kilomita 2.93; umetembelea mradi wa vitalu vya miche ya kahawa katika eneo la Nyamwaga; umezindua kituo cha mafuta cha PKM na mradi wa maji katika eneo la Gamasara.

Mwenge wa Uhuru pia umezindua nyumba tatu za watumishi na kutembelea mradi wa kukusanya mapato kielectroniki katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime; na kutembelea mradi wa barabara ya kilomita moja iliyozinduliwa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2019.

Mwenge wa Uhuru kwa leo unafanya mkesha katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Tarime na kesho utakabidhiwa katika Wilaya ya Rorya kuendelea na mbio zake.

Mbio za Mwenge wa Uhuru zilizinduliwa tarehe 17 Mei 2021 katika Mkoa wa Kusini Unguja  na kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Wiki ya Vijana Kitaifa 2021 itafanyika mkoani Geita tarehe 14 Oktoba 2021.

Katika Mkoa wa Mara Mwenge wa Uhuru unakimbizwa kuanzia tarehe 22 Juni 2021 hadi tarehe 27 Juni 2021 na tarehe 28 Juni 2021 utakabidhiwa katika Mkoa wa Simiyu. 

Kauli mbiu ya mbio maalum za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu “TEHAMA ni Msingi wa Taifa Endelevu: Itumike kwa Usahihi na Uwajibikaji.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa