• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Katibu Tawala awataka watumishi kuwa wabunifu

Posted on: December 16th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya leo ameongoza kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na kuwataka watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara kuwa na mawazo ya ubunifu.  

Akizungumza katika kikao hicho, Bwana Kusaya amewataka watumishi kuongeza ubunifu katika miradi inayotekelezwa na Sekretarieti ya Mkoa na vyanzo vya ukusanyaji wa mapato ya Serikali ili kuboresha huduma kwa wananchi wa Mkoa wa Mara.

“Kwa sasa ukusanyaji wa mapato ya Serikali hauridhishi na kuna huduma muhimu ambazo katika Mkoa wa Mara hazipo, ambazo kama Mkoa tunatakiwa kuhakikisha kutokana na umuhimu wake huduma hizo zinakuwepo” amesema Bwana Kusaya.

Amezitaja huduma hizo kuwa ni pamoja na uanzishwaji wa supermarket kubwa katika Manispaa ya Musoma, kuboresha Ukumbi wa Uwekezaji ili kuweza kutumiwa na watu wengi zaidi na kutafuta wawekezaji waweze kuboresha kantini na klabu zinazomilikiwa na Sekretarieti ya Mkoa.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu, Kaimu Katibu Tawala Bwana Pius Sango Songoma amesema kuwa katika Kipindi cha Julai, 2024 hadi Novemba, 2024 watumishi 44 wamepandishwa vyeo na nane wamebadilishwa vyeo na kurekebishiwa mishahara kwa wakati.

Bwana Songoma amesema katika kipindi hicho watumishi watano hawakuweza kupandishwa vyeo kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutofikisha alama 60 za utendaji kazi kupitia mfumo wa PEPMIS na kuwasistiza watumishi wote kujaza taarifa zao kwenye mfumo huo.

Bwana Songoma amesema ofisi hiyo imeshughulikia mafao ya wastaafu wanne kupitia mfumo wa PSSSF Portal na kuwashauri watumishi kuingia katika mfumo huo na kufuatilia michango yao badala ya kusubiri wanapostaafu.

Aidha, Bwana Songoma amesema katika kipindi hicho Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara wamefanikiwa kupatiwa mikopo ya jumla ya shilingi milioni 350 kutoka Wizara ya Fedha (Hazina) ili kuboresha maisha yao.  

Akitoa elimu kuhusu mgongano wa maslahi Bibi Witness Boniface Msonge Afisa Mwandamizi kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Kanda ya Ziwa amesema katika suala la mgongano wa maadili sio lazima mtu awe amenufaika kiuchumi, wakati mwingine malengo yake mengine yanakuwa yamefikiwa.

Bibi Msonge amesema chanzo cha mgongano wa maslahi ni pamoja na asili ya mwanadamu ambayo ni ya kujipendelea wenyewe na watu wa karibu yake; jukumu ya kijamii yanayohitaji fedha; kulipa fadhili au kuwapendelea ndugu, jamaa na marafiki.

“Wananchi wengi wanaimani kubwa na Serikali na watumishi wa Serikali kuhusu kuwajibika kuwapa huduma bora kwa maslahi yao na Tanzania kwa ujumla” amesema Bibi Msonge na kuwataka wajumbe kutokuivunja imani hiyo ya wananchi.

Bibi Msonge amesema kuna aina tatu za mgongano wa maslahi ambazo ni mgongano halisi wa maslahi ambao unakuwa umetokea, aina ya pili ni hisia za uwepo wa mgongano wa maslahi kutokana na dalili au viashiria mbalimbali, na aina ya tatu ni uwezekano wa kutokea mgongano wa maslahi hapo baadaye.

Bibi Msonge amesema mambo ambayo yanasababisha mgongano wa maslahi ni pamoja na kupokea zawadi, kutumia muda wa ofisi kufanya shughuli binafsi, kufanya biashara kwenye ofisi ambazo mtumishi anaifanyia kazi.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Wakuu wa Idara na Vitengo, Makatibu Tawala wa Wilaya, wawakilishi wa wafanyakazi na wawakilishi vya vyama vya wafanyakazi.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa