• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kamati ya LAAC yahitimisha ziara Mkoa wa Mara

Posted on: March 26th, 2024

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imehitimisha ziara yake ya siku tano katika Mkoa wa Mara kwa kufanya ziara katika Wilaya ya Butiama ambapo pamoja na mambo mengine imetembelea Kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Ikiwa katika Wilaya ya Butiama kamati hiyo imeitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kamgegi na Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama inayoendelea kujengwa katika wilaya hiyo.

Akizungumza katika kikao cha majumuisho, Mwenyekiti wa Kamati ya LAAC Mhe. Stanslaus Mabula ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kutengeneza upya sakafu ya madarasa na milango ya shule hiyo na kuweka mipira chini ya meza na viti ili visiendelee kuharibu sakafu na kumwita Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kukagua.

“Changamoto ninayoiona hapa ni kwamba palikuwa na usimamizi mbovu wa ujenzi tangu fedha zilizopokelewa mpaka sasa, hakukufanyika uchunguzi wa udongo kabla ya kuanza ujenzi, hakukuwa na mpango wa manunuzi katika mradi huu” amesema Mhe. Mabula.

Aidha, Mhe. Mabula amepongeza ujenzi wa nyumba ya walimu (two in one) ambayo amesema imejengwa vizuri kwa vinago vinavyokubalika na ameitaka Halmashauri hiyo kuendelea kutenga fedha kutoka mapato ya ndani ili kukamilisha maabara ya shule hiyo ili wanafunzi waweze kujifunza kwa vitendo.   

Kuhusu Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama Mhe. Mabula ameitaka Ofisi ya Rais TAMISEMI kutoa fedha za ukamilishaji wa hospitali hiyo mapema iwezekanavyo kwa kulingana na hadhi ya hospitali hiyo inayojengwa nyumbani kwa Baba wa Taifa.

“Fedha iliyotolewa katika hospitali hii ni kidogo ukilinganisha na hospitali nyingine za Halmashauri, lakini hapa ni nyumbani kwa Mwalimu Nyerere, panahitaji jicho la kipekee katika kuwapa mgao” amesema Mhe. Mabula.  

Aidha, Mhe. Mabula ameutaka uongozi wa Mkoa wa Mara kuisaidia Halmashauri kumbana mkandarasi aliyepewa kazi ya kujenga jengo la wagonjwa wa dharura (EMD) katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ili arejeshe fedha baada ya kuwa amelipwa fedha yote na mkataba wa kazi hiyo kuvunjwa kabla hajakamilisha kazi katika ujenzi wa jengo hilo.

Akitoa ufafanuzi wa hoja za wabunge kuhusu Shule ya Sekondari ya Kamgegi, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama Bwana Chacha Megewa ameeleza kuwa kabla ya Serikali haijaleta fedha za SEQUIP katika kata hiyo, tayari wananchi wa Kata hiyo walianzisha ujenzi wa madarasa sita na matundu ya vyoo 10 katika eneo hilo.

“Madarasa haya na matundu ya vyoo Serikali kupitia mpango wa lipa kwa matokeo iliyakamilisha na kuanza kutumika isipokuwa madarasa matatu ambayo kwa sasa yanatumika kama stoo ya kuwekea vifaa na jiko la kupikia chakula cha wanafunzi” amesema Bwana Megewa.

Bwana Megewa amewashukuru wananchi wa Kata hivo kwa michango yao ya hali na mali katika ujenzi wa madarasa hayo na matundu 10 ya vyoo ambayo yameongeza miundombinu ya kutolea elimu katika shule hiyo.

Ziara hiyo imehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Katibu Tawala wa Wilaya ya Butiama, wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Butiama, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, maafisa kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.  

Ziara hiyo imehitimishwa kwa wajumbe wa kamati kutembelea Kaburi la Baba wa Taifa katika eneo la Mwitongo, Wilaya ya Butiama kabla ya kuanza safari ya kuelekea Halmashauri ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu kuendelea na ziara yake.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa