• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kamati ya Bunge yaipongeza NHC

Posted on: March 18th, 2020

Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili imelipongeza Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa kazi nzuri waliyoifanya tangu walipokabidhiwa kazi ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara, Rwangwa inayoendelea kujengwa katika Manispaa ya Musoma.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti leo tarehe 17 Machi 2020 wajumbe wa kamati hiyo wamepongeza jitihada iliyofanyika tangu NHC wapewe jukumu hilo hadi sasa.

“Kumekuwa na wakandarasi wengi waliofanya hii kazi tangu hospitali hii ilipoanza kujengwa mwaka 1977 lakini kazi yenu inaonekana, hongereni sana, alisema Mheshimiwa Nape Nnauye, Mbunge wa Mtama.

Wakichangia maoni yao wajumbe wa kamati hiyo wameelezwa kuridhishwa kwao kwa namna hatua ya ujenzi ilipofikia na kazi ambayo NHC kama mkandarasi imefanya katika eneo hilo.

Kwa upande wake, Waziri wa Ardhi Nyumba Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi akizungumza wakati wa utambulisho ameeleza kuwa NHC imekuwa ikifanya vizuri katika miradi yote ya kimkakati iliyopewa.

Ameitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na ujenzi wa machinjio ya kisasa jijini Dar es Salaam, ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara na ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara na mingineyo.

Mheshimiwa Lukuvi amesema mradi huu pia umechelewa kutokana na kuchelewa kupatikana kwa Mshauri Mwelekezi ambaye kwa sasa amepatikana ambaye ni Chuo Kikuu cha Ardhi na anafanyakazi nzuri kwa ushirikiano na NHC.

Hata hivyo amerudia agizo lake la kuitaka NHC kutekeleza ahadi ya kukamilisha upande wenye wodi za Mama na Mtoto na majengo ya mochwari na sehemu ya kufulia katika hospitali hiyo ili ziweze kutumika ifikapo tarehe 17 Aprili 2020.

“Mkurugenzi wa NHC ninaomba kukuambia kuwa kama mradi huu haijakamilika kama tulivyoahidiana ninaomba barua ya kuondoka ofisini uiandike wewe mwenyewe, maana wewe ndio uliahidi utakamilisha ifikapo muda huo” alisema Mheshimiwa Lukuvi.

Wakati huo huo Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Vincent Naano Anney ameipongeza NHC kwa kazi kubwa wanayoifanya hususan ya usimamizi mzuri wa mradi huo.

“Wale wakandarasi wa mwanzo ilikuwa kila siku hapa kulikuwa na kesi za wizi wa vifaa, kwa sasa hamna wizi tena wa kiholelaholela, wanajitahidi sana” alisema Dkt. Anney.

Wakiwa katika eneo hilo wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii walipata nafasi ya kukagua ujenzi wa hospitali hiyo, kupokea taarifa ya ujenzi na kupokea taarifa ya ukaguzi wa mipaka kati ya Kenya na Tanzania.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa