• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kalemani azindua vituo vya mafuta vya serikali

Posted on: June 8th, 2020

Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Medard Kalemani leo tarehe 6 Juni 2020 amezindua vituo vya mafuta vya serikali vyenye lengo la kusogeza huduma za nishati karibu na maeneo ya wananchi.

Akizungumza katika uzinduzi huo mjini Musoma Mheshimiwa Kalemani alisema kwa leo anazindua vituo saba vinavyomilikiwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kupitia kampuni yake tanzu ya TANOIL hapa nchini vikiwa na lengo la kuimarisha na kusogeza huduma za nishati kwa wananchi.

“Serikali imeamua kurudi katika biashara ya mafuta kupitia TPDC na kampuni tanzu ya TANOIL ikiwa ni hatua muhimu kwa usalama na ustawi wa taifa letu” alisema Mheshimiwa Kalemani.

Mheshimiwa Kalemani ameeleza kuwa kwa sasa serikali inazindua vituo saba vya TANOIL nchi nzima na huu ni utekelezaji wa Sera ya Nishati yenye lengo la kupeleka huduma hiyo kwa wananchi.  

Aidha Mheshimiwa Kalemani ameuagiza uongozi wa TPDC kuhifadhi mafuta mengi wakati huu ambako bei ya mafuta duniani imeshuka ili kuweza kuwa na akiba ya kutosha ya mafuta bei itakapopanda katika soko la dunia.

Pia Msheshimiwa Kalemani ameutaka uongozi wa TPDC kufungua vituo vya mafuta viwe vingi hapa nchini ili kuweza kusambaza huduma hizo kwa wananchi walio wengi waweze kunufaika na huduma hizo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amepongeza Wizara ya Nishati kwa kazi kubwa walioifanya ya kurudi katika biashara ya mafuta kupitia TPDC.

“Nilikuwa kiongozi katika Wizara ya Nishati na Madini wakati huo na mpango wa TPDC kurudi katika biashara ya mafuta ilikuwepo ni furaha kuona mipango ile kwa sasa inatekelezwa” alisema Mheshimiwa Malima.

Aidha Mheshimiwa Malima alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli ya serikali nzima kwa kutekeleza suala hili muhimu kwa maendeleo ya Taifa la Tanzania.

Akizungumza wakati wa kutoa taarifa kwa Mheshimiwa Waziri, Mkurugenzi Mkuu wa TPDC Dkt. James P. Mataragio  ameeleza kuwa TPDC inampango wa kushirikiana na Halmashauri zote hapa nchini ili kufungua vituo vya mafuta katika kila halmashauri hapa nchini.

“Kwa kuanzia katika kipindi cha miaka 5 ijayo TPDC inampango wa kufungua vituo vipya 100 vitakavyokuwa katika halmashauri mbalimbali hapa nchini ili kuendelea kusogeza huduma za nishati kwa wananchi. Alisema Dkt. Mataragio.  

Dkt. Mataragio alisema ufunguzi wa vituo hivi utaisaida serikali katika kupanua uwigo wa kodi, kuongeza ubora wa bidhaa, kupanua ajira kwa vijana, na uhakika wa upatikanaji wa mafuta wakati ambapo kuna changamoto.

Ametoa mfano wa miaka ya 1980 TPDC ilikuwa ndio msambazaji mkuu wa mafuta kwa wapiganaji wa msari wa mbele wakati wa vita vya Uganda na Tanzania maarufu kama vita vya Kagera baada ya wasambazaji wengine wa mafuta kugoma kufanya hivyo.

“Kwa niaba ya TPDC ninashukuru sana kwa ushirikiano ambao tumekuwa tukipata kutoka katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara wakati wote tangu vituo hivi vilipojengwa mwaka 1978 hadi sasa” alisema Dkt. Mataragio. 

Shirika la TPDC lilijenga vituo saba vya mafuta katika mikoa ya kimkakati hapa nchini na kufanya biashara ya mafuta kuanzia miaka ya 1978 hadi 2000 TPDC kupitia kampuni yake ya Tipper. Katika Mkoa wa Mara kupitia mpango huo TPDC ilikuwa na vituo vya mafuta viwili ambavyo vipo katika Manispaa ya Musoma na Mji wa Tarime.

Uzinduzi wa kituo cha Mafuta cha TANOIL Musoma ulihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima, Naibu Waziri wa Nishati Mheshimiwa Subira Mgalu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Meya wa Mji wa Musoma na Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma pamoja na viongozi wengine.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa