• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Jafo atoa wiki moja North Mara kuwasilisha taarifa

Posted on: April 22nd, 2021

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mheshimiwa Suleiman Jafo amesikitishwa na ubabaishaji unaofanywa na Mgodi wa North Mara uliopo katika Wilaya ya Tarime, Mkoani Mara katika utekelezaji wa maagizo ya serikali katika kulinda mazingira.

Mheshimiwa Jafo ameeleza masikitiko yake leo tarehe 20 Aprili 2021 wakati akiwa katika ziara ya siku moja Mkoani Mara kutembelea mgodi huo ili kujua hatua za utekelezaji wa maagizo ya serikali.

“Leo mimi nilitegemea wangesema kuwa tumechukua hatua kadhaa na sasa tunategemea kuondokana na tatizo la mlundikano wa maji yenye sumu kwa ifikapo mwezi fulani, lakini haya maelezo yao hayaonyeshi nia ya kuondokana na tatizo hili” alisema Mheshimiwa Jafo.

Kufuatia hali hiyo Mheshimiwa Jafo ametoa siku saba kwa mgodi wa North Mara kuwasilisha taarifa ofisini kwake kuhusu mkataba wao na mkandarasi unaoonyesha ni lini upembuzi yakinifu na muundo wa mfumo mpya wa maji taka utakamilishwa pamoja na mpangokazi wa kutekeleza maagizo ya serikali.  

Mheshimiwa Jafo alisema awali mgodi huu ulikuwa unazalisha maji taka kiasi cha lita za ujazo 7,000,000 kwa sasa wamejitahidi kupunguza wamefikia lita milioni 2.2 hata hivyo bado hayakubaliki kwani Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linataka maji hayo yabakie lita 800,000 ili kulinda afya za wananchi wanaouzunguka mgodi huo.  

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameeleza kuwa suala la kuhifadhi maji machafu ili yasiwaathiri  wananchi limekuwa likiongelewa na serikali kwa muda mrefu lakini mgodi hauchukui hatua za kukomesha hali hiyo.

“Nafahamu kuwa serikali inaubia na mgodi wa Barrick katika uendeshaji wa migodi hii, lakini sisi (serikali) hatuna ubia wowote na mgodi kwenye ulinzi na usalama wa watanzania na mali zao na hatutaki utani kwenye suala nyeti kama hili” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa hata sehemu ambayo North Mara wanasema wameshaitenga kwa ajili ya kujenga bwawa jipya bado mgodi haujalipa fidia kwa wananchi wenye eneo hilo na kama serikali ya Mkoa inasubiri kuona utekelezaji huo.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa hii ni mara ya tatu sasa anafika hapo na mawaziri tofauti wa mazingira kufuatilia jambo hilo lakini wamekuwa wakipewa maelezo ambayo hayaridhishi juu ya utekelezaji wa maagizo hayo.

Awali akitoa maelezo kwa Mheshimiwa Waziri, Msimamizi wa Bwawa hilo Bwana Majuto Kapande ameeleza kuwa kwa sasa upembuzi yakinifu kuhusu mradi huo unaendelea hata hivyo alishindwa kutaja tarehe ya kukamilika kwa upembuzi huo.

“Ni kweli tunalifanyia kazi na kwa sasa tayari mgodi umempa kazi mshauri mwelekezi kutoka Afrika Kusini ambaye anafanya upembuzi yakinifu pamoja na kuandaa michoro na muundo wa bwawa jipya litakalojengwa” alisema Bwana Kapande.

 Hata hivyo Bwana Kapande na wenzake waliokuwa katika msafara huo walishindwa kueleza kuhusu mkataba wao na mkandarasi huyo ulianza lini, unaisha lini na bwawa litaanza kujengwa lini jambo ambalo lilileta wasiwasi kuwa huenda hamna utekelezaji wowote unaoendelea. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa