• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

INEC Yavionya vyama vya Siasa kutokuingilia uboreshaji wa Daftari

Posted on: August 26th, 2024

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) leo tarehe 25 Agosti, 2024 imefanya mkutano na wadau wa uchaguzi Mkoa wa Mara na kuvionya vyama vya siasa kutokuingilia mchakato wa uboreshaji wa Daftari la wapiga kura.

Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo, Mwenyekiti wa Tume Huru la Uchaguzi Jaji Mahakama ya Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amesema mawakala na viongozi wa vyama vya siasa hawaruhusiwi kuingilia mchakato wa uandikishaji vituoni na kufanya hivyo watakiuka Sheria za Uchaguzi.

“Kila Chama cha siasa kimepewa nakala ya orodha ya vituo vyote vya kuandikisha wapiga kura ili kuwawezesha kupanga kupanga na kuweka mawakala wa uandikishaji katika vituo vya kuandikisha wapiga kura” amesema Jaji Mwambegele.  

Mhe. Jaji Mwambegele amevihimiza vyama vya siasa na wadau wa uchaguzi kuzingatia sheria, kanuni za uboreshaji, maelekezo ya Tume na kusimamia miiko na mipaka ya uendeshaji wa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura.

Amevitaka vyama vya siasa kutumia sheria zilizopo kuwasilisha changamoto zinazojitokeza kwa Tume na kuongeza kuwa INEC itazingatia Katiba, Sheria za Uchaguzi na kanuni zilizotungwa chini ya Sheria katika zoezi la uboreshaji.

Jaji Mwambegele amewataka wadau wa uchaguzi kuwa mabalozi wazuri na kutoa taarifa sahihi kwa wananchi na kuwahamasisha wananchi wenye sifa kujitokeza kwa wingi na kuboresha taarifa zao ili zoezi hili lifanyike kwa ufanisi na mafanikio makubwa.

Jaji Mwambegele amesema katika mzunguko wa nne wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura utahusisha mikoa ya Mara, Simiyu, na sehemu ya Mkoa wa Manyara katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati, Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu na Halmashauri ya Mji wa Babati ambapo uboreshaji utaanza tarehe 4-10 Septemba, 2024.

Amesema vituo vya kujiandikisha vitafunguliwa kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni na kuwataka wadau wa uchaguzi katika mikoa hiyo watatakiwa kuwawapa taarifa sahihi wananchi ili waweze kushiriki kikamilifu katika uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uchaguzi INEC Bwana Ramadhani Kailima amesema Tume inategemea vyama vyenye usajiri kamili kutumia fursa za kisheria zilizotolewa kwao kuhakikisha kuwa zoezi la uboreshaji linafanikiwa na kuongeza kuwa endapo kutajitokeza changamoto zozote vyama vitumie taratibu za kisheria zilizopo kuwasilisha hoja zao.

“Viongozi wa vyama vya siasa hawapaswi kuingilia utekelezaji wa majukumu ya watendaji wa vituo wakati wote wa uandikishaji wa wapiga kura vituoni kama kuomba orodha au idadi ya walioandikishwa au kuboresha au kuhamisha taarifa zao” amesema Bwana Kailima.

Bwana Kailima amesema Tume inao wajibu wa kuwapatia viongozi wa vyama vya siasa taarifa kamili ya zoezi la uandikishaji wa Daftari la Wapiga Kura mara baada ya zoezi kukamilika.

Kauli mbiu ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mwaka 2024/2025 ni “Kujiandikisha kuwa mpiga kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora”.

 Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi wa vyama vya siasa, wahariri wa vyombo vya habari za kijamii vilivyopo Mkoa wa Mara, wawakilishi wa makundi mbalimbali katika jamii na wawakilishi wa taasisi za Serikali Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa