• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

IHI kutoa Chanjo ya Kichaa cha Mbwa Mara

Posted on: October 27th, 2023

Taasisi ya Afya Ifakara (IHI) kupitia mradi wake wa utafiti wa kichaa cha mbwa imepanga kuupatia Mkoa wa Mara chanjo ya kichaa cha mbwa kwa muda wa miaka mitano na miundombinu  kwa jumla ya zaidi ya shilingi milioni 400.

Akizungumza wakati wa kuwasilisha matokeo ya awali ya utafiti wa mikakati ya kudhibiti kichaa cha mbwa kwa viongozi na watendaji wa Mkoa wa Mara, Mratibu wa Programu ya Kudhibiti Ugonjwa wa Kichaa cha Mbwa Dkt. Ahmed Lugelo ameeleza kuwa msaada huo ni sehemu ya mwendeleo wa mradi wa kudhibiti kichaa cha mbwa katika Mkoa wa Mara.

“Tutatoa chanjo zenye thamani za zaidi ya shilingi milioni 116 kwa kipindi cha miaka mitano na kwa mwaka huu tutaweka miundombinu yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 279 kwenye kata zilizokuwa kwenye mpango mpya wa majaribio” amesema Dkt. Lugelo.  

Kwa mujibu wa Dkt. Lugelo, chanjo pamoja na vifaa tiba vitaletwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na ofisi hiyo itaratibu zoezi la chanjo hiyo kwa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara  ameseka Dkt. Lugelo.

Dkt. Lugelo ameeleza kuwa tangu mradi huu wa utafiti ulipoanza mwaka 2019, Taasisi ya Afya ya Ifakara kwa kushirikiana na wadau wengine imekuwa ikitoa chanjo ya kichaa cha mbwa katika Mkoa wa Mara bila malipo.

Aidha, Bwana Lugelo ameeleza kuwa wakati wa utafiti huo zaidi ya mbwa 220,000 wamechanjwa katika Mkoa wa Mara na mradi huo pia umetengeneza kifaa cha kuhifadhia chanjo ambacho hakitumii umeme na tayari kimefanyiwa vipimo kinafaa kwa matumizi.

Dkt. Lugelo ameeleza kuwa mradi huo wa miaka mitatu ulianza Oktoba, 2019 na unatarajiwa kuisha tarehe 30 Oktoba, 2023 na umefanyakazi katika Kata 132 katika Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara  

Dkt. Lugelo ameeleza kuwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa unaenea kutoka kwa mbwa kwenda kwa binadamu na wanyama wengine kwa haraka na kwa binadamu chanjo yake inatolewa baada ya mtu kung’atwa na mbwa chanjo hiyo ni ya gharama kubwa na hauna dawa za kuweza kuutibu ugonjwa huo baada ya dalili kuonekana.

Dkt. Lugelo amewashukuru viongozi na watendaji wa Mkoa wa Mara walioshiriki katika kikao hicho na kuwataka watoe elimu kuhusu madhara ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa katika jamii na mwakani mwezi Oktoba, 2023 taasisi hiyo itafanya mkutano wa tathmini kuhusiana na utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa leo.  

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda ameipongeza Taasisi ya Afya Ifakara kwa kuleta mradi huo katika Mkoa wa Mara na kutoa msaada wa chanjo ya Kichaa cha Mbwa pamoja na miundombinu itakayorahisisha udhibiti wa kichaa cha mbwa.  

Mhe. Mtanda amezitaka Halmashauri zote kutafuta namna ya kudhibiti mbwa kuzurura mitaani ili kuondoa hofu kwa wananchi ya kung’atwa na mbwa wenye kichaa cha mbwa.

Kwa upande wao, washiriki wa kikao hicho wameamua kuwa ili kunufaika na msaada huo, Halmashauri zitenge bajeti ya kusaidia kudhibiti kichaa cha mbwa na wananchi wachangie shilingi 500 kwa kila mbwa atakayepatiwa chanjo kwa kipindi hicho.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Meya na Wenyeviti wa Halmashauri, Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Wakurugenzi na watendaji kutoka halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa