• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara kuanza kutoa huduma Aprili 2020

Posted on: March 6th, 2020

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara ya Kwangwa inatarajia kuanza kutoa huduma katika Jengo la Mama na Mtoto kuanzia tarehe 17 Aprili 2020 baada ya kukamilika ujenzi wa upande huo na huduma zote muhimu za kuwezesha kuanza kufanya kazi.

Hayo yameelezwa leo baada ya kikao cha pamoja kati ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kigoma Malima, wawakilishi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambao ndio wakandarasi na mwakilishi wa Chuo Kikuu cha Ardhi ambaye ni Mshauri Mwelekezi katika mradi huo pamoja na maafisa waandamizi wa serikali.

Akizungumza baada ya kikao hicho Mheshimiwa Lukuvi ameeleza kuwa amewaagiza NHC kuhakikisha kuwa wanafanyakazi ya kukamilisha ujenzi wa hospitali hii kwa usiku na mchana na kuhakikisha kuwa huduma zitaanza kutolewa kwa muda uliopangwa.

 “Kwa sasa Mshauri Mwelekezi anarekebisha michoro ya awali ya majengo hayo ili iweze kukidhi mahitaji yote ya msingi ya majengo ya wakati huu” alisema Mheshimiwa Lukuvi.

Kwa upande wake Mheshimiwa Mwalimu amesema kuwa wanategemea kuwa hospitali hii itaanza kufanyakazi kwa kutoa huduma za mama na mtoto na makubaliano ni kuwa hadi kufikia Julai, 2020 hospitali yote itakuwa imekamilika kutoa huduma kwa wananchi.

“Tunategemea kuwa ujenzi huu ukikamilika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara itahamia hapa Kwangwa na pale ilipo sasa yale majengo yatatumika kama Hospitali ya Manispaa ya Musoma” alisema Mheshimiwa Mwalimu

Aidha amesema kuwa hospitali hii haitakuwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa bali itakuwa ni hospitali ya kibingwa na kibobezi kwa baadhi ya huduma na itatoa huduma kwa wananchi wote wa Kanda ya Ziwa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Adam Kighoma Malima amesema kuwa ziara ya viongozi hawa imesadia sana katika kutatua changamoto zilizokuwa zinaukabili ukamilishaji wa hospitali hii. 

Ujenzi wa Hospitali ya Kwangwa ulianza mwaka 1977 na ulikuwa ukijengwa taratibu hadi mwaka 2018 ambapo Rais wa awamu ya tano Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli alipoamua kutoa shilingi bilioni 15 kwa ajili ya kumalizia ujenzi huu.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa