• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hospitali ya Rufaa ya "Kwangwa" kuanza rasmi Julai Mosi

Posted on: June 9th, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu amesema Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara inatarajiwa kuhamia katika majengo ya Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere iliyopo katika eneo la Kwangwa tarehe 01 Julai, 2023.

Akizungumza katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Mara na Wazee wa Manispaa ya Musoma, Bwana Msalika amesema kuhama kwa hospitali hiyo kutatoa nafasi wa majengo yaliyokuwa wakitumiwa na hospitali hiyo kutumika kama Hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Musoma.

“Maandalizi yote muhimu yamekamilika, hospitali ya Rufaa na Hospitali ya Halmashauri zimeshasajiriwa rasmi na zote zipo tayari kwa ajili ya kupokea wagonjwa” amesema Bwana Makungu.

Kwa mujibu wa Bwana Makungu katika kuhakikisha huduma hazisimami katika hospitali ya awali, baadhi ya vifaa tiba, dawa na watumishi wataendelea kubaki kuhudumia wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Musoma ili huduma ziendelee kutolewa.

Aidha, Bwana Makungu amesema tayari Manispaa ya Musoma imepokea fedha shilingi milioni 500 ambazo zitatumika katika kukarabati majengo yaliyokuwa yakitumika na Hospitali ya Rufaa ili yaweze kutumika na Hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Musoma.

Bwana Makungu amewahakikishia wazee wa Manispaa ya Musoma kuwa zoezi la uhamaji limewekewa taratibu ambazo hazitaathiri utoaji wa huduma za Hospitali ya Manispaa ya Musoma wakati kwa hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere maboresho yanaendelea.

Ameyataja maboresho yanayoendelea kuwa ni pamoja na kuboresha upatikanaji wa huduma za maji katika Hospitali ya Rufaa jambo linaloshughulikiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Musoma (MUWASA) na ujenzi wa vyoo vya nje kwa watu wanaokuja kuona wagonjwa vinavyosimamiwa na Shule ya Sekondari ya Ufundi ya Musoma.

Wakati huo huo, Bwana Makungu amesema iliyokuwa Musoma Hoteli inatarajiwa kufufuliwa baada ya mwekezaji mwenye asili ya Mkoa wa Mara kuonyesha nia ya kutaka kuwekeza katika Hoteli hiyo.

Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Musoma Mhe. Magiri Benedicto Malegesi ameitaka Serikali kukipanua Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare ili kiweze kuchukua programu nyingi na kutoa shahada za kwanza.

“Kwa sasa Chuo kina wanafunzi 900 tu, wakiongeza michepuo na wakianza kutoa Shahada kitaongeza idadi ya wanafunzi na hilo litaisaidia sana katika kukua kwa Manispaa ya Musoma” alisema Mhe. Malegesi.

Mhe. Malegesi ameiomba Serikali kufufua viwanda vya zamani na kujenga viwanda vipya ili kuongeza  ajira kwa wananchi wa Mkoa wa Mara.

Wengine walioshiriki katika mazungumzo hayo Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Afya, Ustawi wa Jamii na lishe Dkt. Zabron Masatu, Meya wa Manispaa ya Musoma Mhe. Wiliam Gumbo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma Bwana Bosco Ndunguru.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa