• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hospitali ya Rufa ya Mkoa wa Mara yaanza kutoa huduma

Posted on: September 1st, 2020

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara ambayo ni maarufu kuwa Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere iliyojengwa katika eneo la Kwangwa, Manispaa ya Musoma imeanza kutoa huduma kwa wananchi leo tarehe 31 Agosti 2020.

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameeleza kuwa kuanza kutolewa huduma katika hospitali hii ni uthubutu wa serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dokta John Pombe Joseph Magufuli aliyetoa msimamo wa kukamilishwa kwa hospitali hii.

“Hospitali hii ilikuwa inajengwa tu awamu zote tangu mwaka 1977, lakini kwa sasa serikali imeamua kuikamilisha na imekamilika na leo imeanza kutoa huduma kwa wananchi, tunashukuru sana” alisema Mheshimiwa Malima.

Kwa mujibu wa Mheshimiwa Malima kwa sasa Hospitali hiyo imeanza kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje (OPD) na Kitengo cha Mama na Mtoto. Aidha ukamilishaji wa shughuli zilizosalia unaendelea ili kuweza kufungua Kitengo cha Magonjwa ya Ndani na kuanza kusafisha figo katika hospitali hii.

“Sisi kama Mkoa tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa uwekezaji mkubwa alioufanya ili kulinda afya za wananchi wa Mkoa wa Mara na maeneo jirani” alisema Mheshimiwa Malima.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Florian Tinuga ameeleza kuwa tayari serikali imeongeza watumishi wengi wa sekta ya afya wakiwemo madaktari ili kuwezesha hospitali hii kuanza kutoa huduma kikamilifu.

“Awali Mkoa ulikuwa na madaktari 34 mwaka 2015 na sasa wameongezeka hadi kufikia madaktari 102 mwaka 2020 na kati ya hao sita ni madaktari bingwa” alisema Dokta Tinuga.

Dokta Tinuga ameeleza kuwa serikali ya awamu ya tano imekamilisha pia hospitali nne za halmashauri za wilaya ambazo ni za halmashauri za wilaya ya Serengeti, Musoma Vijijini, Rorya na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda. Aidha serikali imejenga vituo vya afya nane katika Mkoa wa Mara.   

Kwa upande wake mmoja wa wazazi ambaye amejifungua mtoto wake katika hospitali hii Bibi Lucy Msela Nzunda mkazi wa mkazi wa Makoko, alimshukuru Mungu kwa kujifungua salama.

Bibi nzunda amesema huduma katika hospitali hii ni nzuri na wauguzi wamempa ushirikiano na amefurahi sana kuwa mama wa kwanza kujifungua mtoto katika hospitali hii ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.  

Wazo la kujenga hospitali hii lilitolewa na Mwalimu Nyerere mwaka 1975 na ujenzi wa hospitali hii ulianza mwaka 1977 na ulifanywa na wakandarasi mbalimbali na baadae kusimama hadi mwaka 2018 baada ya serikali ya Awamu ya Tano kutoa fedha shilingi bilioni 15 kwa ajili ya kukamilisha hospitali hii.

Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ni kati ya Hospitali 10 za rufaa zilizokamilishwa na serikali ya awamu ya tano kwa usimamizi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika kipindi cha miaka mitano.

Tayari mpaka jana mchana akinamama watatu walikuwa wamejifungua watoto salama katika hospitali hiyo ambapo watoto wawili walikuwa wakike na mmoja wa kiume.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa