• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hoja zenye Jinai zipelekwe kwenye vyombo vya dola

Posted on: July 22nd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kujibu hoja zote za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ndani ya mwezi mmoja na zile zenye sura ya jinai ndani yake zipelekwe kwenye vyombo vya dola.

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo hayo leo tarehe 14 Julai, 2022 katika kikao maalum cha Baraza la Madiwani la halmashauri hiyo kwa ajili ya kujadili hoja za CAG.

“Hapa tunahoja nyingi ambazo zinajinai ndani yake, sasa tukishindwa kuzijibu tuvikabidhi vyombo vya dola vizishughulikie na wahusika warejeshe pesa ya Halmashauri iliyotumika vibaya” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha ameitaka Halmashauri hiyo kuwashtaki watumishi waliokuwa wanakusanya mapato bila ya  kupelekwa benki; waliopewa masurufu ambao wameshindwa kurejesha; walioandika hati kwa mkono kuficha GFS Code; na  waliofanya matumizi yasiyo sahihi.   

“Ninataka mzabuni aliyelipwa shilingi 292 kwa ajili ya kuleta vifaa vya ujenzi wa ofisi za Halmashauri ambaye hajaleta kwa muda mrefu na waliohusika wote wachukuliwe hatua za kisheria” aliagiza Mheshimiwa Hapi.

Aidha, ameitaka Halmashauri hiyo kuongeza nguvu katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri na kusema “sijaridhika kabisa Halmashauri hii kuishia asilimia 70 ya makusanyo ya ndani, ongezeni juhudi ili miradi ya wananchi iliyopangwa iweze kutekelezwa kwa ufanisi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa kuongeza wafanyakazi katika Idara ya Mipango mapema iwezekanavyo.

Kwa upande wake, mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Bunda Bibi Changwa Mkwazu ameeleza kuwa Halmashauri hiyo ilipata hati mbaya katika taarifa kuu, hata hivyo bado haijapokea taarifa ya mradi wa mfuko wa pamoja wa afya (Health Basket Fund).

Bibi Mkwazu ameeleza kuwa halmashauri ilikuwa ina hoja 92 na kati ya hizo hoja 49 ni za miaka ya nyuma wakati hoja 43 ni za mwaka wa fedha 2020/2021.

Bibi Mkwazu ameeleza kuwa kati ya hoja za miaka ya nyuma kuanzia mwaka wa fedha 2012/2013 ambapo hoja 04 zimejibiwa na kufungwa, hoja 16 zipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji wakati hoja 29 hazijatekelezwa.

Katika hoja za mwaka wa fedha 2020/2021, Bibi Mkwazu ameeleza kuwa hoja 08 zimejibiwa na kufungwa, hoja 27 zipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji, hoja 07 hazijatekelezwa wakati hoja moja imepitwa na wakati.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mheshimiwa Charles Manumbu ameeleza kuwa Halmashauri hiyo imechukua hatua za kuimarisha makusanyo ya mapato ya ndani na sasa inakusanya vizuri.

Mheshimiwa Manumbu ameishukuru Serikali kwa kubadilisha watumishi waliokuwa wamekaa muda mrefu na kuwaleta wengi wapya, hata hivyo ameiomba Serikali kuongeza watumishi katika Idara ya Mipango ya Halmashauri hiyo.

 “Ni matumaini yangu, mwakani Halmashauri hii itapata hati safi baada ya wataalamu wengi waliokuwepo kubadilishwa na waliokuja kuonekana wanafanya kazi vizuri” alisema Mheshimiwa Manumbu. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa