• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi: Mkawatumikie Wananchi

Posted on: June 22nd, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 21 Juni 2021 amewaapisha Wakuu wa Wilaya wanne wapya walioteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan tarehe 19 Juni 2021.

Akizungumza wakati wa kuawaapisha wakuu wa wilaya hao, Mheshimiwa Hapi amewataka kwenda kusimamia miradi ya serikali inayotekelezwa katika wilaya zao ili wananchi waweze kupata manufaa ya miradi hiyo kama ilivyokusudiwa.

“Wananchi  wamekipa dhamana Chama cha Mapinduzi (CCM) wakiamini kitawaletea maendeleo na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili na CCM ikaunda serikali ya Rais aliyewatuma kumwakilisha huku kutatua kero za wananchi wa Mkoa wa Mara, sasa tukachape kazi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amewataka Wakuu wa Wilaya kutumia asimilia 70 ya muda wao wakiwa kwenye kukagua miradi na kusikiliza kero za wananchi na kutumia asilimia 30 tu ya muda wao kukaa ofisini.

“Ninataka mtenge muda na siku maalum mkiwa na wataalamu wenu ili kusikiliza kero za wananchi wa wilaya zenu na kutatua baadhi ya kero za wananchi mtakazoweza na ambazo mtaona mnahitaji msaada kuzitatua tupo tayari kusaidiana kuweza kuzitatua ” alisema Mheshimiwa Hapi.   

Aidha Mheshimiwa Hapi amewataka viongozi hao kusimamia haki za wananchi wanyonge pamoja na watumishi waliopo katika maeneo yao hususan wanaoishi maeneo ya vijijini .

“Mhakikishe kuwa Maafisa Utumishi wanaenda kuwasikiliza watumishi mbalimbali waliopo katika maeneo yenu,  ili watumishi wawatumikie wananchi wakiwa na furaha na wananchi nao wahudumiwe wakiwa na furaha” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amewataka kutilia mkazo zaidi katika sekta za huduma za jamii hususan elimu, afya, maji na umeme ambazo zinawaathiri wananchi wangi katika maeneo yao. 

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela amewapongeza Wakuu wa Wilaya hao kwa kuaminiwa na Mheshimiwa Rais ili waweze kusimamia wilaya hizo.

Aidha amewataka Wakuu wa Wilaya hao kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo katika utendaji kazi wao ikiwemo ya utoaji wa taarifa nje ya Mkoa.

“Ninawaomba mkawatumie vizuri wataalamu na vyombo vya ulinzi na usalama vilivyopo chini yetu kwa ajili ya kuwashauri na kuwapa utaalamu unaohitajika katika utekelezaji wa majukumu yenu” alisema Bwana Msovela.

Wakuu wa Wilaya walioapishwa leo ni Mheshimiwa Dkt. Vincent Mashinji  kuwa Mkuu wa Wilaya ya Serengeti;  Mheshimiwa Juma Issa Chokoka kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rorya; Mheshimiwa Joshua Samweli Nassari Mkuu wa Wilaya ya Bunda na Mwalimu Moses Rudovick Kaengele Mkuu wa Wilaya ya Buatiama.

Wengine ambao Mheshimiwa Rais amewahamishia katika Mkoa wa Mara ni Mhe. Dkt. Halfan Haule Mkuu wa Wilaya ya Musoma na Lt. Col. Michael Mangwela Mtenjele Mkuu wa Wilaya ya Tarime. 

Shughuli ya uapisho huo umehudhuriwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara Mheshimiwa Samweli Kiboye, Viongozi wa Dini, Makatibu Tawala wa Wilaya, Meya wa Mji wa Musoma, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri pamoja na watumishi , viongozi wa taasisi mbalimbali za serikali na za binafsi pamoja na wananchi wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa