• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi awashukuru Wasabato kwa kusistiza Chanjo ya UVIKO 19

Posted on: November 5th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara amelipongeza Kanisa la Waadventista Wasabato kwa kuwapa elimu ya UVIKO 19 waumini wao na kuwasistiza kuchanja Chanjo ya UVIKO 19 ili kupunguza makali ya ugonjwa huo.

Mheshimiwa Hapi ameeleza hayo leo tarehe 09 Oktoba 2021 katika eneo la Nyamongo Wilayani Tarime ambapo alikuwa mgeni rasmi katika kufunga mkutano na mahubiri ya AMANI ITOKAYO JUU yaliyokuwa yakirushwa moja kwa moja kwa waumini wa dhehebu hilo duniani kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii ya kanisa hilo.

“Nimefurahi sana kusikia kuwa mlipokuwa hapa mmepata elimu juu ya UVIKO na chanjo ya UVIKO 19 na walioweza wamechanja, ninawapongeza sana” alisema Mheshimiwa hapi.

Amewahakikishia waumini wa dhehebu hilo kuwa chanjo ya UVIKO 19 ni salama na lengo la serikali kuileta nchini ni kupunguza athari za ugonjwa huo kwa wananchi wake.

Mheshimiwa Hapi amelishukuru Kanisa hilo kwa kuisaidia serikali katika kutoa huduma za afya na elimu katika Mkoa wa Mara na maeneo mengine hapa nchini.

Mkuu wa Mkoa amelihakikishia Kanisa hilo ushirikiano kutoka kwa watendaji na viongozi wa serikali katika Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Jimbo la Kaskazini mwa Tanzania Mchungaji David Makoye ameeleza kuwa katika Mkutano huo uhamasishaji wa chanjo ya UVIKO 19 ulifanyika na waumini walipata huduma ya kuchanja kwa hiari baada ya kupewa elimu kuhusu chanjo ya UVIKO 19.  

“Mkutano huu umesaidia sana waumini waliotaka kuchanjwa wamechanjwa hata ambao hawakutaka kuchanjwa wamepewa elimu kuhusu UVIKO 19 na umuhimu wa chanjo hiyo” alisema Mchungaji Makoye.

Mchungaji Makoye ameeleza kuwa katika mkutano huo huduma mbalimbali za afya zimetolewa ikiwa ni pamoja na uchunguzi na tiba ya afya ya kinywa na meno, macho, kugawa mewani, uchunguzi wa magonjwa yasiyoambukizwa kama vile kisukari, shinikizo la dam una uzito uliokithiri.

Aidha alieleza kuwa katika mkutano huo elimu ya afya ya kinywa na meno ilitolewa kwa wanafunzi wa darasa la pili wa shule ya Msingi Kewanja na wanafunzi hao pia awaligawiwa dawa za meno na miswaki 300.

Mchungaji Makoye alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuja kufunga mkutano huo uliodumu kwa siku 21 ambao ulihusisha kanisa lote yaani majimbo Makuu mawili ya Kaskazini na Kusini mwa Tanzania la Kanisa la Waadventista Wasabato.

Ameeleza kuwa Jimbo la Mara lipo chini ya Jimbo Kuu la Kaskazini mwa Tanzania na limeundwa na Mkoa mmoja wa Mara pamoja na Wilaya ya Ukerewe iliyopo katika Mkoa wa Mwanza na linajumla ya waumini 334,561 kwa sasa.

Mchungaji Makoye ameeleza kuwa Jimbo la Mara linaunga mkono juhudi za serikali kwa kutoa huduma katika sekta ya afya, elimu na huduma nyingine za kijamii.

Kwa upande wa Elimu jimbo la Mara linamiliki shule nane ambazo ni Shule ya Sekondari ya Ikizu, Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Busegwe, Shule ya Sekondari ya Bwasi, Shule ya Seondari ya Nyansincha, Shule ya Sekondari ya Nyabohore na Shule ya Sekondari ya Kameya.

Mchungaji Makoye amezitaja shule nyingine kuwa ni Shule ya Msingi Murderspach pamoja na Hope International School. 

Aidha ameeleza kuwa Jimbo la Mara linatoa huduma za afya kupitia zahanati 04 zinazomilikiwa na Kanisa hilo ambazo ni Zahanati ya Kamunyonge, Tarime, Bukwe na Nansio.

Mchungaji Makoye ameeleza kuwa katika mkutano huo, ulikuwa na vipindi mbalimbali ambavyo vilihusu masuala ya Watoto, ambacho kililongelea malezi kwa Watoto kiroho, kimwili, kiakili na kijamii; afya na familia ambacho kilizugumzia unyumba bora wenye mafanikio, kupunguza migogoro katika familia na jamii; afya kilizungumzia afya tiba, kinga, kutoa elimu dhidi ya mila na desturi zinazokinzana na maadili mema katika jamii.

Aidha kipindi cha neno la Mungu kilizungumzia malezi ya kiroho, kuwaandaa watu kuwa raia wema hapa duniani na katika ufalme ujao pamoja na kuombea amani Taifa letu na pia.

Mahubiri katika mkutano huo yametangazwa katika eneo la Nyamongo, kitaifa na kimataifa kupitia televisheni, radio na mitandao ya kijamii ya kanisa hilo baada ya kutafsiriwa katika lunga za Kiingereza, Kifaransa, Kiarabu, Kireno na lugha ya alama kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum.

Katika msafara wake Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara Mheshimiwa Samweli Kiboye (Namba 3) na Mkuu wa Wilaya ya Tarime Kanali Michael Mtengele.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa