• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi awapongeza wananchi wa Kirumi

Posted on: November 5th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amewapongeza wananchi wa eneo la Kirumi katika wilaya ya Butiama kwa kuanzisha ujenzi wa Zahabati ya Kirumi ambayo sasa serikali imeongeza fedha za kupanua kuwa Kituo cha Afya.

Mheshimiwa Hapi ametoa pongezi hizo leo tarehe 8 Oktoba, 2021 katika eneo hilo baada ya kugagua maendeleo ya ujenzi na kupatiwa taarifa ya maendeleo ya mradi huo.

“Mimi niwapongeze sana kwa jitihada zenu za kubuni na kuanzisha mradi huu ambao sasa serikali unaenda kuupanua ili huduma zote muhimu ziweze kupatikana hapa” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amemwagiza Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kuwa katika jengo la awali, chumba cha kujifungulia na wodi ya waliojifungua viongezwe ukubwa ili kukidhi mahitaji.

MKuu wa Mkoa pia amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Butiama kusimamia vizuri utekelezaji wa miradi hiyo ili kuendana na matamanio ya Serikali ya Awamu ya Sita katika mradi huo.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa fedha iliyoletwa Kirumi ni sehemu ya shilingi 1,550,000,000 zilizoletwa katika Mkoa wa Mara kwa ajili ya kujenga vituo vya afya katika Wilaya ya Serengeti, Butiama, Rorya, Bunda na Tarime.

Ameeleza kuwa Wilaya ya Butiama imepata bahati ya kupata vituo viwili ambapo kuna Kituo cha Kirumi kilichopata milioni 300 na Kituo cha Afya Makongoro kilichopata milioni 250 katika mgao huo.

Mheshimiwa Hapi amewataka wahusika wa mradi huo kuusimamia vizuri ili uweze kuleta matokeo yanayotarajiwa na serikali ya awamu ya sita.

“Ninawapongeza sana kwa kuanza kujenga shule ya msingi mpya katika eneo hili ambayo itawasaidia Watoto kupata elimu karibu na mazingira yao, Mkurugenzi fuatilia maendeleo ya ujenzi na halmashauri ikamilishe ujenzi wa shule hiyo na isajiriwe” alisema Mheshimiwa Hapi.

Akitoa taarifa ya mradi huo, Mtendaji wa Kijiji cha Kirumi Bi. Vailet Francis Kisumo ameeleza kuwa mradi wa ujenzi wa zahanati hiyo ulianza mwaka 2010 kwa nguvu za wananchi.

“Halmashauri ya Wilaya ya Butiama iliongeza shilingi milioni 128 kwa nyakati tofauti ili kuweza kukamilisha jengo hilo” alisema Bi. Kisumo.

Bi, Kisumo ameeleza kuwa kwa sasa Kijiji cha Kirumi kimepokea shilingi milioni 300 kutoka serikalini kwa ajili ya kukamilisha jengo hilo pamoja na kujenga kichomea taka na maabara.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa