• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi awapongeza Wanamara

Posted on: February 17th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amewapongeza wananchi wa Mkoa wa Mara kwa ushirikiano, utulivu, uzalendo na mshikamano walioionyesha wakati wote ambapo Mkoa ulipata ugeni mkubwa wa viongozi wa Chama cha Mapinduzi na Serikali walioshiriki katika maadhimisho ya miaka 45 ya CCM na ziara ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  

Akizungumza katika kikao cha tathmini ya miradi ya maendeleo kilichofanyika leo tarehe 15 Februari 20222 katika ukumbi wa uwekezaji uliopo katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Hapi amesema wananchi walionyesha uzalendo wa hali ya juu.  

“Wananchi walihakikisha kuwa ziara ya Mheshimiwa Rais inafanyika kwa amani, utulivu na hamasa kubwa sana, kwa niaba ya viongozi wote wa Mkoa wa Mara ninawapongeza sana” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka wananchi kuendelea na uzalendo huo kwa manufaa ya wananchi wenyewe lakini na taifa kwa ujumla.

Aidha amevipongeza vyombo vya usalama kwa kusimamia amani na utulivu katika maeneo yote ya Mkoa wa Mara na kuhakikisha wageni wote wanarudi majumbani kwao wakiwa salama.

Mheshimiwa Hapi pia amewashukuru wafanyabiashara wa Mkoa wa Mara ambao walitoa huduma mbalimbali kwa wageni waliokuja na kuujengea sifa Mkoa wa Mara.

“Wafanyabiashara wengi waliitikia wito wa kufanya biashara zao saa 24 kwa siku ambazo wageni walikuwepo katika Mkoa wa Mara, hii ilisaidia kutoa huduma kwa wageni ambao walichelewa kufika na ambao walihitaji kuamka mapema kuwahi sehemu mbalimbali.

Aidha, Mheshimiwa Hapi amewataka wafanyabiashara wa Mkoa wa Mara kuendelea kuboresha huduma katika biashara zao kwa kuwa wageni wameondoka na sifa nzuri za Mkoa wa Mara wengine watapenda kuja tena wakati mwingine wakute huduma bora zaidi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kujitokeza kwa wananchi kwenye mikutano na maeneo ambayo Mheshimiwa Rais alikuwa anapita ni ishara nzuri kuwa wananchi wengi wanaipenda serikali yao.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alifanya ziara ya siku nne katika Mkoa wa Mara ambapo alikuwa Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya miaka 45 ya Uhuru, aliweka jiwe la msingi katika mradi wa maji wa Mgango- Kiabakari- Butiama, alitembelea Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (Kwangwa) na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa maji Bunda.

Aidha katika ziara hiyo Mheshimiwa Rais alizungumza na wananchi katika Uwanja wa Karume uliopo Manispaa ya Musoma, eneo la Mgango, Kwangwa, Butiama na Mji wa Bunda.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Rais pia alitembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika eneo la Mwitongo ambapo pamoja na mambo mengine alizuru na kuweka Shada la Maua katika kaburi la Baba wa Taifa.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa