• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi awaongoza Wananchi Kusherekea Muungano

Posted on: April 26th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara leo amewaongoza wananchi wa Wilaya ya Musoma kupanda miti 1,000 katika Shule ya Sekondari ya Kiara kama sehemu ya Maadhimisho ya miaka 58 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Akizungumza baada ya zoezi la upandaji miti, Mheshimiwa Hapi amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kupanda miti ili kulinda mazingira ya Mkoa wa Mara kwa ajili ya vizazi vijavyo.

“Miti hii ambayo kivuli chake tunakipata leo, ilipandwa na wazee wetu hapo zamani na sasa ni wajibu wetu kupanda miti na kutunza mazingira” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka wanafunzi na walimu wa shule zote za Mkoa wa Mara kupanda miti katika maeneo yao ili kulinda uoto wa asili wa Mkoa wa Mara.

Akitoa shukrani kwa Mkuu wa Mkoa, Meya wa Manispaa ya Musoma Mheshimiwa William Gumbo ameeleza kuwa Shule ya Sekondari ya Kiara imechaguliwa kuzindua zoezi la upandaji miti kutokana na sababu za kihistoria.

“Serikali ilipoanza kujenga shule za kata, shule ya kwanza kujengwa na wananchi wa Manispaa ya Musoma ilikuwa ni Sekondari ya Kiara, mwitikio ulikuwa mkubwa sana na nguvu za wananchi zilifanikisha ujenzi wa shule nzima ndani ya muda mfupi” alisema Mheshimiwa Gumbo.

Mheshimiwa Gumbo ameeleza kuwa hata zoezi hili la upandaji wa miti linaweza kufanikiwa sana kutoakana na uzoefu huo na mwitikio wa wananchi katika ujenzi wa Shule hiyo.

Mstahiki Meya amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuungana na wananchi wa Manispaa ya Musoma kupanda miti kama sehemu ya uzinduzi wa kampeni ya kupanda miti 30,000 katika Manispaa ya Musoma.

Mheshimiwa Gumbo ameeleza kuwa zoezi la kupanda miti katika Manispaa ya Musoma ni endelevu na kuwataka wanafunzi na wananchi kuchukua miche ya miti katika kitalu cha Wakala wa Misitu (TFS) Manispaa ya Musoma na kupanda katika maeneo yao.

Zoezi la kupanda miti lilihudhuriwa pia na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Katibu Tawala wa Wilaya ya Musoma, Wakuu wa Idara na Vitengo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, wakuu wa taasisi za serikali na wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Wengine waliohudhuria ni Meya wa Manispaa ya Musoma, Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma, Wakuu wa Idara na Vitengo vya Manispaa ya Musoma na watumishi wa Manispaa ya Musoma, wanafunzi na walimu wa Shule ya Sekondari ya Kiara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa