• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi atoa wiki mbili kwa mkandarasi kuilipa Halmashauri

Posted on: July 25th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amemtaka mkandarasi wa mradi wa barabara ya Butiama- Makutano kulipa deni Service Levy analodaiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ndani ya wiki mbili.

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo hayo wakati leo tarehe 19 Julai 2021 alipokuwa katika ziara ya siku moja katika Halmashauri ya Wilaya ya Butiama katika mradi wa barabara wa Butiama- Makutano.

“Nenda ukalipe pesa zetu shilingi zaidi ya milioni 80 ndani ya wiki mbili ili halmashauri iende kutekeleza miradi ya maendeleo ya wananchi” amesema Mheshimiwa Hapi.

Aidha amemuagiza Meneja wa TANROADS Mkoa wa Mara kuhakikisha mkandarasi anafanyakazi kwa haraka kukamilisha barabara hiyo ambayo inaingia eneo la Butiama hadi nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na maeneo mengine katika Wilaya ya Butiama.

Katika mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara amepiga marufuku mkandarasi kutumia kokoto, kifusi na mchanga wa kujengea kutoka mikoa mingine na kuamuru atumie zinazotoka katika Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Butiama Mheshimiwa Jumanne Sagini ameeleza kuwa ujenzi wa barabara hiyo umechukua muda mrefu sana, barabara hii ina urefu wa kilometa 50 lakini ujenzi wake umechukua muda wa zaidi ya miaka sita mpaka sasa.

“Jambo hili linawakera wananchi kwa sababu barabara nyingine za urefu huu zinakamilika wakati hii inakuwa inaendelea kujengwa bila sababu za msingi” alisema Mheshimiwa Sagini.

Ameeleza kuwa wananchi wa Butiama walikuwa wamesikitika sana baada ya mkandarasi kuleta kokoto na malighafi za kujengea barabara hiyo kutoka Mkoa wa Geita, na kuwa anashukuru jambo hilo kwa sasa mkandarasi amelirekebisha.

“Tunafurahi kama ameanza kuchimba kokoto hapa kwa sababu kwanza ataipatia halmashauri yetu mapato lakini pili vijana wetu watajipatia ajira kwenye maeneo haya” ameeleza Mheshimiwa Sagini.

Mheshimiwa Sagini ameeleza kuwa vipande vya barabara vilivyobakia kati ya Butiama na Makutano ni kero kubwa sana kwa wananchi wa Butiama kwani inasababisha barabara hii ionekane haiishi kwa muda mrefu sana. 

Aidha Mheshimiwa Sagini ameeleza kuwa wananchi pia wanalalamikia suala la ulipaji wa fidia kwa baadhi ya nyumba zilizokuwepo katika eneo la barabara na malipo yao yapo na wananchi ambao hawajachukua fidia zao waende wakachukue kwenye ofisi za TANROADS Mkoa wa Mara. 

Akitoa maelezo ya mradi huo, Mshauri Mwelekezi katika mradi huo ameeleza kuwa ujenzi wa barabara hiyo ulianza rasmi mwaka 2013 na wakati unaanza kulikuwa na vitu vingi ambavyo vilikuwa havijakaa sawa na hivyo kusababisha changamoto katika utekelezaji wa mradi huo.

“Mshauri Mwelekezi alikuwa hajapatikana na ilichukua takriban miezi sita kumpata na baadaye alipokuja lilijitokeza tatizo kuwa mradi haukuwa sawasawa, Mshauri mwelekezi alilifanyiakazi na ilichukua muda mrefu baadaye kufanyia kazi changamoto mbalimbali za mradi kabla ya mradi kuanza kutekelezwa” alisema Mshauri Mwelekezi.

Mshauri Mwelekezi ameeleza kuwa kwa sasa mradi umekuwa unakwama kutokana na mkandarasi JV constructions Limited kutegemea fedha anayolipwa ndio aendelee na kazi na malipo yakikwama na kazi inakwama. Mshauri Mwelekezi ameeleza kuwa kwa sasa mkandarasi amelipwa kiasi cha bilioni 1.7 na kazi imeanza tena kutekelezwa.

Mshauri Mwelekezi ameeleza kuwa kwa sasa mradi huo ambao unatengenezwa kwa gharama ya bilioni 60 unatarajiwa kukamilika tarehe 15 Desemba 2021 na mpaka sasa kazi hiyo imekamilika kwa asilimia 89.

Ameeleza kuwa ujenzi wa madaraja yote ya mradi huo yamekamilika kilichobakia ni vipande vya barabara ambavyo bado hajakamilisha kulingana na michoro na makubaliano ya mkataba.

 Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Butiama, viongozi wa taasisi za serikali na viongozi wengine.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa