• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi atoa mwezi mmoja kukamilisha vyoo Sekondari ya Buturi

Posted on: July 16th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ametoa mwezi mmoja Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya akamilishe ujenzi wa choo katika Shule ya Sekondari ya Buturi iliyopo katika Mji wa Shirati.

Akizungumza katika mkutano wa wananchi katika Mji wa Shirati leo tarehe 15 Julai 2021 Mheshimiwa Hapi amepokea malalamiko kutoka kwa mwananchi kuhusu shida ya vyoo inayowakabili wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Buturi.

“Ninatoa mwezi mmoja hadi tarehe 15 Agosti 2021 choo cha Sekondari ya Buturi kiwe kimekamilika na kinahudumia wanafunzi wa shule hiyo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha Mheshimiwa Hapi ameagiza kuacha mara moja kutoza shilingi 2,000 kwa wafanyabiashara wa chakula kwa ajili ya fomu ya kupima afya na badala wake wafanyabiashara wapatiwe fomu hiyo wakatoe nakala.  

Mkuu wa Mkoa wa Mara alitoa maagizo hayo kufuatia Bwana Musa Mbogo kueleza kero ya choo katika Sekondari ya Katuru na jitihada ambazo wananchi walizifanya kunusuru hali hiyo.

Bwana Mbogo ameeleza kuwa baada ya wananchi kuona wanafunzi wa shule hiyo hawana choo walichangia kuchimba shimo, matofali na fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa choo hicho lakini fedha hizo kiongozi mmoja wa mtaa aliyehusika katika kuzikusanya amekimbia nazo.

Aidha Bwana Mbogo ameeleza kero nyingine kuwa ni zahanati ya eneo hilo ambayo ilikuwa inajengwa kwa nguvu za wananchi ambayo imesimama kwa muda mrefu bila taarifa za kueleweka.

Akitoa majibu ya kero hiyo Mtendaji wa Kata hiyo alieleza kuwa ni kweli wanachi walichangia nguvukazi, matofali na fedha kujenga choo na mhusika ametoroka na fedha hizo na kwa sasa kesi imelipotiwa polisi na mtuhumiwa bado anaendelea kutafutwa.

Aidha Mtendaji wa Kata alieleza kuwa kwa sasa walimueleza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Rorya ambaye aliahidi kutoa fedha kukamilisha ujenzi wa choo hicho.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya ameeleza kuwa alipewa taarifa na watendaji, alitenga shilingi milioni 3 ambazo zitakuja kukamilisha Chuo hicho.

Aidha katika mipango ya muda mrefu Halmashauri kwa kutumia bajeti ya 2021/2022 imetenga milioni 25 kutoka mradi wa P4R kwa ajili ya kujenga vyoo vingine katika Shule ya Sekondari ya Buturi.

Aidha Mkurugenzi aliahidi kufuatilia fedha shilingi 2,000 ambayo ilikuwa inatozwa na Afisa Afya kwa wafanyabiashara wa chakula kama ilikuwa inaingia kwenye mfuko wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

Katika mkutano na wananchi uliofanyika katika Mji wa Shirati, Mkuu wa Mkoa alitoa nafasi kwa wananchi kueleza kero zao na kuuliza maswali ambayo yalikuwa yanajibiwa na waatendaji mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

Mkuu wa Mkoa wa Mara alifanyaziara ya siku moja katika Wilaya ya Rorya na Tarime kukagua miradi ya Maji na mpaka wa Tanzania na Kenya katika wilaya hizo na aliongea na wananchi katika maeneo mbalimbali.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi afungua kambi ya madaktari bingwa na bobezi 64 Mara

    June 23, 2025
  • Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara wapatiwa mafunzo

    June 20, 2025
  • Mara mshindi wa pili UMITASHUMTA 2025

    June 18, 2025
  • Zingatieni miongozo ya kilimo cha tumbaku- Dkt. Haule

    June 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa