• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi Ataka Wakandarasi wawajibikaji

Posted on: June 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi katika Mkoa wa Mara kuwajibika kwa mujibu wa mikataba yao na kukamilisha miradi kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma.

Akizungumza katika kikao na wakandarasi wote wanaotekeleza miradi katika Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Hapi amewakumbusha wakandarasi kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia mikataba yao bila kusukumwa na wasimamizi wa miradi hiyo.

“Haiwezekani mkandarasi umeomba kazi, umepewa, sasa kutekeleza hadi uitwe na polisi na usimamiwe ili utekeleze mradi ulioomba wewe mwenyewe, hiyo haikubaliki” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ametoa mwezi mmoja kwa wakandarasi wa miradi ya barabara zinazosimamiwa na TARURA na TANROADS wanaolalamikiwa kuchelewesha miradi kuikamilisha miradi hiyo.

Mheshimiwa Hapi amewataka wasimamizi wa wakandarasi na wakandarasi wote kuheshimu mamlaka za serikali katika ngazi za Mkoa, Wilaya ya Halmashauri wanazofanyiakazi na kutoa ushirikiano kwa viongozi wa mamlaka hizo katika kutekeleza miradi ya waanchi.

Aidha Mheshimiwa Hapi amewataka Wakuu wa Wilaya kusimamia na kuhakikisha wanapata taarifa za miradi yote inayotekelezwa na mamlaka mbalimbali katika maeneo yao.

“Wakuu wa Wilaya msikubali taasisi na wakandarasi waende kukabidhiana miradi gizani bila ya uwepo wa wananchi na viongozi katika makabidhiano ya miradi hiyo, daini taarifa” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka wakandarasi wote kulipa ushuru wa huduma (service levy) kwa Halmashauri kutokana na kazi wanazozifanya katika Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara Bwana Langaeli Akiyoo ameeleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameleta fedha nyingi za kutekeleza miradi katika Mkoa wa Mara lakini miradi hiyo mingi haitekelezwi vizuri.

“Tulipita kukagua miradi ya maendeleo, miradi mingi ipo chini ya kiwango au utekelezaji hauendani na michoro ya awali (BOQ) ya mradi husika hususan miradi ya barabara” alisema Bwana Akiyoo.

Aidha Bwana Akiyoo amewataka wakandarasi kufanyakazi kwa ushirikiano na viongozi waliopo katika maeneo miradi inapotekelezwa. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wakandarasi wa Mkoa wa Mara Mhandisi Municali Mseti amewataka wakandarasi kutekeleza majukumu yao ya kitaaluma kwa weredi na kwa wakati.

“Ukandarasi ni biashara ya kitaaluma, ambayo kutoifanya vizuri kunaidhalilisha taaluma hii ya uhandisi ambayo wengi wetu tumeisomea na tunaifanyia kazi” alisema Bwana Mseti.

Aidha Bwana Mseti ameiomba serikali kuwalipa wakandarasi kwa wakati pale wanaokuwa wanadai baada ya kufanyakazi zao.

Kabla ya kufunga kikao hicho wakandarasi wote wamekula kiapo cha kutekeleza majukumu yao vizuri na kutii mamlaka za Serikali zilizopo katika maeneo wanapotekeleza mradi yao.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Meya na Wenyeviti wa Halmashauri, wakuu wa taasisi, mwenyekiti wa Jumuiya ya Wandandarasi na wakandarasi wenyewe. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa