• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi ataka ubora katika utekelezaji wa afua za lishe Mara

Posted on: February 17th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuchukua hatua za maksudi kuboresha utekelezaji wa afua za Lishe ili kuboresha lishe ya wananchi wa Mkoa wa Mara. 

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo hayo wakati wa kikao cha tathmini ya masuala ya lishe kilichofanyika leo katika ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Haiwezekani kadi alama ya lishe kwa kipindi cha nusu mwaka bado inaonyesha Mkoa wa Mara tupo kwenye alama nyekundu katika kutoa fedha na katika kuweka katika bajeti fedha inayohitajika kwa kila mtoto wa chini ya umri wa miaka mitano” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuwachukulia hatua Maafisa Lishe na watendaji wengine wote wanaokwamisha utekelezaji wa afua za lishe katika Mkoa wa Mara.

“Kila mtu awasimamie watu wa eneo lake na wakichukuliwa hatua ushahidi ubaki katika mafaili yao ili kuhakikisha kuwa kazi zinafanyika kwa ufanisi, weredi na uzalendo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameagiza vikao vya tathmini ya masuala ya lishe kufanyika katika ngazi za Halmashauri na Wilaya mwishoni mwa mwezi Machi, 2022 ili mapungufu yanayoonekana yafanyiwe kazi kabla ya kuletwa katika kikao cha tathmini ya lishe kwa ngazi ya Mkoa.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuangalia uwezekano wa kuingiza fedha za miradi ya wadau wa maendeleo katika bajeti zake ili ziweze kutumika pamoja na mambo mengine kutekeleza masuala ya afua za lishe.

Awali, taarifa ya utekelezaji wa afua za lishe, Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kwa kipindi cha kuanzia Julai, 2021 hadi Desemba, 2021 zilitenga fedha chini ya asilimia 50 inayohitajika lakini hata kiasi hicho cha fedha kilichotengwa pia kilitumika kwa kiasi kidogo au hakikutumika kabisa katika kipindi hicho. 

Aidha, katika taarifa hiyo, Halmashauri nne hazikutenga pesa wala hazikutumia pesa kabisa katika kipindi hicho cha tathmini, Halmashauri hizo ni Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Mnispaa ya Musoma, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Wakitoa maelezo kuhusiana na hali hiyo, wakurugenzi wa Halmashauri zote wamekiri kutenga na kutumia fedha ambazo zilitokana na wadau wa maendeleo na fedha za mapato ya ndani lakini hazikuonekana kwenye mfumo wa lishe kutokana na kuwa hazikuingizwa kwenye bajeti ya Halmashauri au zilitumika baada ya tarehe 15 Desemba, 2021 na hivyo kutoonekana katika tathmini ya wakati huu badala yake  zitaonekana katika kipindi kijacho cha tathmini.

 Kikao cha tathmini ya afua za lishe katika Mkoa wa Mara kimehudhuliwa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Bwana Benjamini Oganga, Wakuu wa Wilaya, Mganga Mkuu wa Mkoa, Wakuu wa Idara za Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Wakurugenzi wa Halmashauri, Waganga Wakuu wa Halmashauri na Maafisa Lishe wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa