• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi ataka maelezo ujenzi wa choo Kituo cha Afya Changuge

Posted on: July 26th, 2021

HAPI ATAKA MAELEZO UJENZI WA CHOO KITUO CHA AFYA CHANGUGE

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Rorya Bwana Charles Chacha Marwa na timu yake kutoa maelezo ya matumizi ya shilingi milioni 22 kujenga choo katika Kituo cha Afya cha Changuge kilichopo katika Halmashauri hiyo.

Mheshimiwa hapi ametoa maagizo hayo leo tarehe 23 Julai 2021 wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara ilipotembelea na kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM katika halmashauri hiyo.

“Haiwezekani choo hiki chenye matundu sita kutumia milioni 22 wakati sehemu nyingine tunajenga tundu moja la choo kwa shilingi milioni 1,100,000 tu lakini hapa fedha hii ni kubwa sana na sisi hatujaridhika na kazi hii” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amemtaka Mkurugenzi kuambatana na wahusika wote katika mradi huo na kuwasilisha maelezo yao kesho tarehe  24 Julai 2021 saa nne kamili.

 “Mje na mambo mawili, maelezo au fedha zilizobakia katika maradi huo…..nikiona jinai nitatoa maagizo kwa Jeshi la Polisi liwaweke ndani na kupelekwa mahakamani” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kumpangia majukumu mengine Mganga Mfawidhi wa Kituo hicho Dkt.  Respicous  Rugemalila na kuondoa uongozi wote wa kituo hicho baada ya kukuta mazingira machafu katika kituo hicho.

 “Chama na Serikali hatujaridhika na mazingira ya kituo hiki, ni pachafu na hii sio sawa kabisa, huwezi kuwa na kituo cha afya kichafu namna hii halafu watu wamekaa tu hapa” alisema Mheshimiwa Hapi.

Ametoa mwezi mmoja kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kuhakikisha kuwa anaunganisha mfumo wa mapato ya serikali (GOTHOMIS) katika kituo hicho ili kudhibiti mapato ya serikali.

Mkuu wa Mkoa amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kuwasismamisha kazi watumishi ambao walikuwa zamu zamu wakati vifaa vinaibiwa na kuwafungulia mashauri ya kiutumishi kulingana na makosa yao kiutumishi na kuhakikisha kuwa vifaa vinapatikana na visipo patikana wakatwe mishahara yao kufidia hasara hiyo.

Mheshimiwa Hapi amemuagiza Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Kipolisi Utegi kuchunguza upya wizi wa vifaa katika kituo hicho unaorudia rudia mara kwa mara.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara Mheshimiwa Samweli Kiboye ameeleza kuwa chama kimepokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi kuhusiana na Kituo cha Afya Chenguge.

Ameeleza kuwa Chama cha Mapinduzi hakijaridhishwa na matumizi ya fedha hiyo yote katika mradi huo wa Choo.

“Hii hospitali ni ya siku nyingi sana na CCM tumepiga kelele sana, tunashukuru sana kwa hatua ulizozichukua leo na Chama kipo nyuma yako, na Chama hakijaukubali mradi huu” Mheshimiwa Kiboye.

Mheshimiwa Kiboye ameeleza kuwa Kituo hicho ni kichafu sana na hakina maji ya uhakika na wagonjwa wanakuja na maji yao.

Aidha Mheshimiwa Kiboye ameeleza kuwa kuna vifaa vya maabara vimeibiwa tarehe 8 Machi 2021 katika hospitali hiyo na kuongeza kuwa kituo hicho kimekuwa kikiibiwa vifaa mara kwa mara na wizi wa mwezi Machi  ni mara ya sita tangia uanze wizi huo.

Kamati ya siasa katika Wilaya ya Rorya ilitembelea pia mradai wa vijana wa bodaboda, Shule ya Sekondari Nyanduga, mradi wa ujenzi wa barabara, Hospitali ya Wilaya ya Rorya na Kituo cha Afya Changuge.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa