• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi ataka elimu zaidi ya kodi

Posted on: June 14th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuongeza utoaji wa elimu kwa wananchi na wafanyabiashara kuhusiana na masuala ya kodi ili waweze kuilipa kwa hiari.

Mheshimiwa Hapi ameeleza hayo leo tarehe 14 Juni, 2022 wakati wa kikao cha Jukwaa la Wadau wa Kodi la Mkoa wa Mara ambalo limefanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Kama tulivyosikia katika majadiliano hapa, wafanyabiashara wanataka wanataka kulipa kodi tatizo wanakosa elimu kuhusiana na aina ya biashara wanayoifanya na kodi wanazotakiwa kulipa” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameishauri TRA kuandaa vipeperushi vinavyozungumzia aina za biashara na kodi wanazotakiwa kulipa katika biashara hiyo ili kuwarahisishia wafanyabiashara kuweza kujua kwa wakati wanachotakiwa kulipa kama kodi kwa serikali.

Aidha ameishauri TRA kuunda makundi sogozi (whatsap groups) ya wafanyabiashara wa aina moja ili kuyatumia makundi hayo kubaini kama kuna changamoto na elimu inayohitajika kwa wafanyabiashara wa aina hiyo na kutatua kero zao mara moja.  

“Wafanyabiashara wengi hawana elimu ya biashara na kodi, hivyo ili kukusanya kodi kwa utaratibu mzuri TRA inapaswa kuwaelimisha wananchi kuhusu biashara wanazofanya, kodi wanazotakiwa kulipa na matumizi ya kodi hizo katika kuboresha huduma za jamii” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa elimu ya kutosha ikitolewa mara kwa mara itawafanya wananchi kuona fahari katika kulipa kodi n ahata kuwachagua viongozi ambao hawana tabia za kukwepa kulipa kodi kwa serikali.  

Aidha ameishauri TRA kufanya utafiti zaidi kuhusu kuongeza wigo wa kodi ili watu wengi zaidi waweze kulipa kodi ili kuongeza mapato ya Serikali na hatimaye serikali kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mheshimiwa Hapi amemuagiza Katibu Tawala Msaidizi, Uchumi na Uzalishaji Dkt. Noel Komba kuhakikisha Maafisa Biashara wa Halmashauri za Mkoa wa Mara wanawasaidia wafanyabiashara katika kukuza biashara zao kwa kuwapa elimu na ushauri kuhusu biashara zao.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewataka wafanyabiashara kukataa kuwa sehemu ya wafanyabiashara wachache wanaokwepa kulipa kodi halali na kuwataka wakibaini watoe taarifa kwa mamlaka zinazohusika.

Kwa upande wake Meneja wa TRA Mkoa wa Mara Bwana Adam Ntoga ameeleza kuwa majukwaa ya kodi yapo katika mikoa yote Tanzania Bara yenye lengo la kupata mrejesho kutoka kwa wadau wa kodi utakaosaidia kuboresha huduma na kuongeza uhuari wa kulipa kodi.

Bwana Ntoga ameeleza kuwa madhumuni ya kuanzisha baraza hili ni pamoja na kuwezesha majadiliano kati ya TRA na wadau wa kodi ili kuimarisha usimamizi wa kikodi; kushauri juu ya muundo na utekelezaji wa mkakati wa malengo ili kufanikisha dira na dhamira ya mamlaka, kupitia na kuboresha taratibu za kodi ziendane na mazingira ya biashara na kubadilisha mawazo juu ya mifumo ya huduma iliyomo ndani ya mamlaka na kupendekeza namna nzuri ya utoaji wa huduma kwa walipa kodi.

Madhumini mengine ni kutoa maoni na mapendekezo kwenye mpango wa TRA wa kuwaelimisha walipa kodi; kupitia na kupendekeza mabadiliko kwenye sheria na kanuni za kodi, pamoja nan jia za kupambana na ukwepaji wa kodi; kuwasilisha maboresho yoyote yenye lengo la kufanikisha dhumuni la kuanzishwa kwa jukwaa la wadau.

Bwana Ntoga ameeleza kuwa kwa mujibu wa sheria, vikao vya Jukwaa la Wadau wa Kodi vinafanyika mara mbili kwa mwaka.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa